Social Icons

Wednesday, 20 January 2016

Watu 62 wanamiliki nusu ya utajiri wa dunia

Matajiri zaidi 62 duniani, hivi sasa wanamiliki zaidi ya nusu ya utajiri wa wakaazi wote wa dunia, limesema shirika la hisani la Oxfam, kuelekea mkutano wa kiuchumi wa dunia - World Economi Forum (WEF) Davos, Uswis.

Davos Weltwirtschaftsforum 2016

Ripoti hiyo ya Oxfam inasema utajiri wa watu hao 62 matajiri zaidi umeongezeka kwa asilimia 44 tangu mwaka 2010, huku utajiri wa watu maskini zaidi bilioni 3.5 umeshuka kwa asilimia 41. Ripoti hiyo iliyopewa kichwa cha habari kisemacho: "Uchumi wa asilimia 1", inabainisha kuwa wanawake wanaathirika zaidi na ukosefu wa usawa duniani.

Karibu nusu ya matajiri zaidi wa dunia wanatokea nchini Marekani, 17 barani Ulaya na waliosalia wanatoka katika mataifa yakiwemo China, Brazil, Mexico, Japan na Saudi Arabia.

Moja ya mambo muhimu yaliyoainishwa katika ripoti ya Oxfam ambayo yanayochangia ukosefu wa usawa duniani ni kupungua kwa mgao wa pato la taifa linalokwenda kwa wafanyakazi karibu katika mataifa yote yalioendelea na yanayoendelea, na kuongeza kuwa wengi wa wafanyakazi wanaolipwa kiasi kidogo zaidi cha mshahara ni wanawake.

Wanaharakti wa Oxfam wakiwa wameva vikaragis vya baadhi ya viongozi wa Dunia watakaoshiriki mkutano wa WEF.

Wanaharakti wa Oxfam wakiwa wameva vikaragis vya baadhi ya viongozi wa Dunia watakaoshiriki mkutano wa WEF.

Pengo la walio na wasio nacho lazidi kupanuka

Ingawa viongozi wa dunia wamezidi kuzungumzia haja ya kukabiliana na ukosefu wa usawa, Oxfam inasema pengo kati ya matajiri zaidi na wengine limetanuka zaidi katika kipidi cha miezi 12 iliyopita.

Utabiri wa Oxfam, yaliyotolewa siku moja kuelekea mkutano wa Davos wa mwaka jana - kwamba asilimia moja ya matajiri zaidi wa dunia watamiliki zaidi ya sisi sote tuliobakia katika muda usiyo mrefu, ulitimia mwaka 2015, imeongeza ripoti hiyo.

Wakati idadi ya watu wanaoishi katika hali ya umaskini uliyokithiri ilipingua kwa nusu kati ya mwaka 1990 na 2010, wastani wa kipato cha asilimia 10 ya watu maskini zaidi duniani umeongezeka kwa chini ya dola tatu kwa mwaka katika kipindi cha robo karne iliyopita, hili likiwa ongezeko la chini ya senti moja katika kipato cha mtu mmoja mmoja kwa mwaka.

Zaidi ya wakuu 40 wa nchi na serikali watahudghuria mkutano wa Davos unaoanza Jumanne jioni na kumalizika Januari 23. Taarifa ya awali iliyotolewa na waandaji wa mkutano huo wa uchumi duniani, ilisema mkutano huo wa ngazi ya juu unaofanyika katika eneo la mapumziko la Davos nchini Uswisi watahusisha pia viongozi wapatao 2,500 wa kibiashara na kijamii.

Mwasisi wa mkutano wa WEF, Mjerumani Klaus Schwab.

Mwasisi wa mkutano wa WEF, Mjerumani Klaus Schwab.

Mapinduzi ya nne ya kiviwanda

Akifafanua kuhusu kaulimbiu ya mwaka huu -- Mapinduzi ya nne ya kiviwanda -- mwasisi wa WEF Klaus Schwab amesema inamaanisha kuunganisha teknolojia katika ulimwengu wa kimaumbile, kidigitali na kibayolojia, ambako kunaanzisha uwezo mpya kabisaa na kuathiri mifumo ya kisiasa, kijamii na kiuchumi.

Mkurugenzi mkuu wa shirika la Oxfam Winnie Byanyima, ambaye anahudhuria mkutano wa Davos baada ya kuwa mwenyekiti mwenza wa mkutano wa mwaka uliyopita, alisema haikubaliki kwa nusu ya watu maskini zaidi wa dunia kumiliki siyo zaidi ya matajiri zaidi wachache, ambao wanaweza kuingia katika basi moja.

Utajiri wa Afrika nje

Kama kipaumbele, Oxfam inataka kukomeshwa kwa enzi ya maeneo salama ya kodi, ambao yameshuhudia ongezeko la matumizi ya vituo vya nje kukwepa kulipa kodi. "Hili linazinyima serikali rasilimali muhimu zinahitajika kupambana na umaskini na ukosefu wa usawa," inasema ripoti hiyo.

Karibu asimilia 30 ya utajiri wa kifedha wa Afrika unakadiriwa kushikiliwa nje ya bara hilo, iliongeza ripoti hiyo, na hivyo kugharimu takribani dola bilioni 14 katika mapato yanayopotezwa kila mwaka.

Wanaharakati wa Oxfam wakiandama kupinga ukosefu wa usawa wa kiuchumi.

Wanaharakati wa Oxfam wakiandama kupinga ukosefu wa usawa wa kiuchumi.

Kufikia viwango sahihi vya kodi kutakuwa muhimu ikiwa viongozi wa dunia watafikia malengo yao, waliojiwekea mwaka uliyopita, ya kufuta kabisaa umaskini uliyokithiri ifikapo mwaka 2030.

Byanyima aliwapa changamoto washiriki wa mkutano wa Davos kutoa mchango wao katika kukomesha enzi ya maeneo salama ya kodi, ambayo yanachochea ukosefu wa usawa wa kiuchumi na kuwazuwia mamia ya mamilioni ya watu kujiondoa katika umaskini.

Miongoni mwa watu 62 wanaosemekana kumiliki utajiri sawa na asilimia 50 ya maskini zaii, Oxfam ilisema 53 ni wanaume na tisa tu ndiyo wanawake, hii ikionyesha kuwa hata kwenye ngazi za juu wanawake wanawakilishwa vibaya.

Mwandishi: Iddi Ssessanga/afpe,rtre
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman

Chanzo. Dw.de

Hadithi: Usilie Nadia: 20



“Jonas, sijui kama utamuona mama yako tena. Nasema sijui kwa sababu anajua mwenyewe ni wapi alipo. Hautakaa utulie tena maana utaandamana na mwenye laana Nadia, hautatabasamu tena kwasababu upo na nyumba ya kilio Nadia, hautakuwa na uhuru kwa sababu upo na mfungwa Nadia. Lakini kikubwa amini kuwa huyu mfungwa atakufa naye atakuacha, lakini hatakufa kizembe kama mmama yako, hatashikika kipuuzi kwa mapenzi na kubwa zaidi akifa atakuacha ukiwa katika mikono ya yeyote yule ambaye hajalaaniwa.

 Utamuita mama naye atakuita wewe mtoto wake. Sitakuacha Jonas hadi roho yangu itakapouacha mwili!!!” nilizungumza na kitoto kile kilichokuwa kinanitazama tu bila kusema chochote!!


Asubuhi nilikuwa mkimbizi kuelekea mahali pengine!! Mwanza haikunifaa tena, mropokaji aitwaye Jesca angeweza kunichoma. Nikazima simu yangu na kusahau kabisa kama niliwahi kuwa na simu!!!”…akasita Nadia akatazama kushoto na kulia.

“Wee G hapa huwa pabaya usiku wanakaba sana mwenzangu na hii afya yangu mgogoro wasije wakaniua bure….” Kauli hii ikanishtua, kweli palikuwa na giza na tulikuwa tumebaki watu wachache sana, tukasimama na kujikongoja tukapata teksi kwa ajili ya kuturudisha hotelini.
Kila mmoja alikuwa kimya!!

Nilikuwa na swali moja kubwa. Nadia alisema kuwa hatamwacha Jonas hadi yeye afe kwanza, sasa mbona Jonas hayupo na yeye yupo hai??
Nini kilitokea na kusababisha haya!!!
Na nini hatima ya Jesca…….

Tulifika hotelini, nikatarajia Nadia atakuwa amechoka na atahitaji kulala moja kwa moja. Lakini haikuwa kama nilivyotarajia, badala yake akaungana nami katika chumba changu kwa mara ya kwanza tangu tuwe katika hoteli ile ya G G jijini Mwanza.
“Nikajua unaenda kulala.” Nikamwambia, hapo akanitazama kisha akanieleza kuwa hakuwa na usingizi wa kulala mapema kiasi kile.
“Usingizi nilikuwa nao enzi zile lakini sasa hapana, yaani usingizi kitu cha ajabu mfano unakuwa unahitaji kulala lakini hauupati, na ukiwa na mambo ya msingi ya kufanya nd’o unakuandama. Leo nilitaka kulala mapema lakini ndo basi tena.” “Au kibaridi hiki kinakusumbua?” nilimuuliza huku akiwa amekaa kitandani nami nikiwa katika kiti.

“Hii nayo utaiita baridi, achana na Mbeya na Iringa. Kuna baridi kali sana kule, hili linaweza kuitwa joto na mtu anayetoka huko. Mara yangu ya kwanza kwenda niliteseka sana, na hata nilipokuja kuzoea nilikuwa nimesota haswa. Halafu bora basi ningeteseka peke yangu, mbaya zaidi nilikuwa na mtoto, mtoto asiyejua kusema badala yake analia tu. Unashindwa kuelewa kuwa huyu anahisi baridi ama ana njaa ama anaumwa, yaani nilikuwa najikuta nalia wakati mwingine, mbaya zaidi ya yote Nadia mimi sikuwahi hata kulea mtoto asiyekuwa wangu. Na kubwa zaidi sijawahi kuwa mama. Labda nililaaniwa hivyo ili laana ya mama iishie kwangu tu isimwandame na mtoto ambaye nitamzaa. Sasa nilikuwa na mtoto mdogo.

Mama Aswile hakujali kama nilikuwa nina mtoto, alinilaza katika chumba kisichokuwa na chandarua na mbaya zaidi hata chakula kilikuwa kidogo sana na kisichostahili kuliwa na mtoto mdogo. Sikuweza kujilaumu kwa kuwa katika mkoa wa Mbeya bali nilijilaani tu kwa nini nilizaliwa.
Lakini zaidi nilimlaumu Jesca ambaye sikujua kama yu hai ama ni marehemu tayari, bila Jesca kunisaliti wala tusingekuwa hapo lakini Jesca akaendekeza mapenzi na hatimaye kilio kinakuwa cha mtoto, unadhani ghafla kiasi kile ningewezaje kupata akili ya ghafla ya kujua nini natakiwa kufanya?, mjini Musoma nilijua hapanifai ikiwa sijajipanga, Mwanza ndo hivyo Bryan atakuwa ananisaka, Dar es salaam napo hapakunifaa maana ndo yalikuwa makazi ya Bryan, hivyo nikajikuta katika sintofahamu. Nikaendelea kuishi na Bryan pale nyumba ya kulala wageni kwa siku zaidi ya tatu na hapo nikawa nimeamua kwenda katika wilaya ya Magu nje kidogo ya jiji la Mwanza. Na hapa nikaendelea kuitwa Maria mama mama Jonas.
Huku nilifikia nyumba ya kulala wageni na kisha nikawa nazurura na Bryan nikitafuta walau kazi za ndani ilimradi nipate sehemu ya kulala bure huku nikitafakari nini cha kufanya na pesa yangu ambayo ilikuwa inayoyoma.
Labda ningekuwa peke yangu ningeweza kwenda Musoma ama popote na kujificha nikifanya lolote niweze kula, lakini sasa nilikuwa na mtoto. Mtoto ambaye nilimuapia kuwa sitamwacha pekee hadi nife. Kiapo changu kikawa kinaniandama na kunifanya nijilazimishe kuizoea hali.
Nikabahatika kupata kazi katika banda la mama ntilie maarufu wilayani Magu, Mama Ntuzu. Nilimweleza shida yangu akanielewa na hapo nikaanza rasmi kushughulika katika banda lake, uzuri wa Jonas kama nilivyokwambia awali hana tabia ya kuchagua nani ambebe na nani asimbebe, yaani halii hovyo. Akilia ujue kuna jambo linamkabili. Hivyo nilikuwa namkabidhi kwa mtu ananisaidia kumbeba iwapo anataka kulala, na wakati mwingine anajumuika na watoto wenzake katikia kucheza, hapo akiwa na miaka takribani miwili.

Tatizo lilikuwa moja tu, kwa siku nilikuwa nalipwa shilingi elfu tatu na bado nilikuwa naishi nyumba ya kulala wageni, hapo nilikuwa nalipia chumba shilingi elfu tatu pia. Hivyo pesa yangu yote ilikuwa inaishia katika nyumba za kulala wageni.

Muda si mrefu nikapata rafiki akanieleza kuwa anaishi peke yake, akanizoea nikamzoea na mwisho akanikaribisha kwake. Kilikuwa chumba kimoja, nikajitoa mhanga nikamnunulia Jona kigodoro chake halafu mimi nikawa nalala na Hamida katika godoro moja. Hamida hakuwa mtu wa makuu, aliniheshimu nami nikamuheshimu na ni huyu aliyeniunganisha na mzee Aswile ambaye alinichukua hadi jijini Mbeya kwa ajili ya kufanya kazi za ndani. Nilimweleza kuwa nina mtoto lakini hakujali kuhusu hilo alionekana kumwamini sana Hamida ambaye alikuwa amempa sifa kemkem kuhusu mimi. 

Nikaagana rasmi na Hamida nikatoweka nikiambatana na mzee Aswile kuelekea Mbeya. Tulisafiri kwa kutumia gari lake binafsi, nilikuwa najiuliza maswali kwanini mzee yule atoke mbali kote huko na mwisho kunichukua mimi kwa ajili ya kumfanyia kazi za ndani lakini sikupata majibu. Nafsi yangu ilikuwa na amani zaidi kuishi mbali na sehemu zote ambazo nilikuwa na mikasa, na Mbeya ilikuwa sehemu nzuri zaidi.

Nilipokelewa kwa furaha na familia nzima, wakazoea kuniita dada, mama mwenye nyumba alikuwa kama mama yangu nilimweshimu na yeye akanionyesha heshima waziwazi.Mtoto wa Jesca ambaye alihesabiwa na kutambulika kama mtoto wangu alikuwa na furaha kama amezaliwa katika familia hiyo.

Tukuyu ikanizoea na mimi nikaizoea. Nikanawiri na kujiona mwanadamu mwenye baba na mama pamoja na wadogo na dada zangu. Familia ya mzee Aswile ikawa kama nyumbani nilipozaliwa.

Raha zile zikanifanya nisahau tetesi ambazo aliwahi kuniagusia mvulana wa kazi kuwa mzee Aswile na mkewe hawana maelewano mazuri sana baada ya mimi kufika pale, mkewe alikuwa akimtuhumu kuwa yule Jonas anayeaminika kuwa ni mtoto wangu, basi nilizaa na mzee Aswile tuhuma ambazo mzee Aswile alizikataa na kisha kumkanya mkewe asije akanibughuzi.

 Aliniambia pia kitu ambacho nilikuwa sikijui, kumbe wale watoto wote pale nyumbani si wa mama yule, bali mama wa wale watoto alikufa katika mazingira ya kutatanisha na mama huyu wa sasa hakubahatika kupata mtoto.
Niliyapuuzia na kuyasaha maneno yale hasahasa baada ya kijana yule kunitaka kimapenzi, hivyo nikagundua kuwa kumbe ile ilikuwa janja yake tu ya kunishawishi.
Maisha yakaendelea na yakasahaulika aliyonambia kijana yule, sikuona chuki yoyote kutoka kwa yule mama na familia nzima ilinipenda.

Jonas akamzoea sana mzee Aswile naye mzee akawa anamfanyia mambo ambayo hata watoto wake baadhi hakuwa akiwafanyia. Niliifurahia sana familia ile, lakini sikujua kama itafika siku ya mimi kuanza kulia tena na kuishi kama mkimbizi.

Usiku huu Jonas alikuwa mtu wa kulialia na kukosa raha, nilishangazwa sana na hali hiyo, si mimi hata mtoto mmoja wa mzee Aswile aliyekuwa anapenda sana kunitembelea chumbani kwangbu alishangaa, hatimaye akasinzia. Lakini saa tisa usiku akaamka tena na kuanza kulia huku akijinyonganyonga huku na kule, nikastaajabu, haikuwa kawaida hata kidogo kwa Jonas. Nikamuuliza alichokuwa anataka, sasa aliweza kusema neno moja tu ‘babuuu’ alikuwa akimtaka babu yake, nikajua ni mambo ya watoto haya kulilia hata visivyowezekana, nikambembeleza sana mwisho akalala, lakini hakudumu sana akaamka tena na kuendelea kunisumbua. Sasa nikaamini Jonas atakuwa anaumwa, nikafikiria kuwa pakikucha niangalie utaratibu wa kumpeleka hospitalini.

Kilio cha Jonas cha saa kumi na moja mara kikaambatana na kilio kingine kutoka kwa mtu nisiyemfahamu, mara mwingine na mwingine na hatimaye mimi naye nikaungana nao.
Tuliongana kumlilia mzee Aswile, kwani hakuweza kuamka tena tangu alivyolala usiku. Mzee Aswile alikuwa amekufa!!

Mwandishi, nililia sana lakini sikumfikia Jonas ambaye ni kama alijua jambo lililotaka kutokea tangu usiku wa manane. Mzee Aswile akazikwa huku tukisema kuwa sisi ni mavumbi na mavumbini tutarudi. Na hapo ukaanza ule wakati wa kujuta na kishga kukumbuka kuwa umelaaniwa, wakati wa kuyakumbuka maneno ya ‘;shamba boy’ juu ya yule mama. 

Ulianza ugeni, wakaja ndugu wa yule mama. Nikatolewa katika chumba nilichokuwa na lala na kisha kuhamishiwa chumba cha nje. Mara kila mara kugombezwa hata ninapofanya jema, baadaye inavyoonekana watoto walihoji kulikoni. 

Naam!! Yule mam akawaambia kuwa baba yao alikufa kwa kulishwa sumu, na chakula hicho nilikipika mimi, nilimlisha sumu ili Jonas aweze kurithi mali. Kwa kuwa wote walikuwa wasichana basi Jonas ambaye ni mtoto haramu ninayemsingizia kuwa wa marehemu angeweza kurithi mali zote. Maneno hayo aliniambia mtoto mkubwa wa marehemu siku moja baada ya kukasilishwa na uwepo wangu sebuleni, alisema kwa uchungu na kisha akaniita shetani. Mama mwenye nyumba alikuwa amewajaza sumu watoto wale.

Hapo sasa nikaanza kuchukiwa!!
Nikabaini kuwa nilibweteka na sikuwa na utaratibu wa kujitunzia pesa, nilijiona kama nipo nyumbani kwetu. Pesa ya nini?? Chumba nilichohamishiwa hakikuwa na kitanda na enzi za uhai wa Aswile katika chumba kile bata na kuku wagonjwa walitengwa na wengine kwa kuhifadhiwa ndani ya chumba kile.

Niatakiwa kuishi mule, ni hapo nikagundua kuwa sikuwa na ile thgamani tena iliyokuwepo awali. Maneno ya shamba boi yakaendelea kujirudia kichwani mwangu, nikajua moja kwa moja kuwa mama yule alikuwa amemuua mumewe kutokana na wivu mzito wa kimapenzi. Lakini nani angeniamini iwapo nilikuwa nimerushiwa kesi ile.

Ugumu wa maisha ukaanzia hapo, nikahesabiwa siku niwe nimeondoka pale. Nikaomba nipewe mwezi mmoja. Hakika ulikuwa mwezi mmoja lakini ni kama mwaka mzima kwa tabu nilizopitia. Nilitukanwa mimi na Jonas, tulilishwa makapi, sikuruhusiwa kuingia sebuleni na mbaya zaidi sikutakiwa hata kupika chakula. Watoto wakadai nitawaua wao pia.

Wakavuka mipaka wakaanza kumuita Jonas mwanaharamu. Hapo sasa wakaitibua hasira yangu na kunirudisha miezi kadhaa nyuma miezi ambayo hasira ilikuwa kando nami na iliweza kufanya kazi muda wowote.
Jonas mwanaharamu!!!

Monica, mtoto mkubwa wa marehemu mzee Aswile alikuwa wa kwanza kutambua upande wa pili wa Nadia. Siku hiyo Jonas akiwa mtoto hajui kama tumekatazwa kuingia sebuleni aliingia na kujibweteka katika kochi akawa anaangalia luninga, mimi nilikuwa nafua nguo zake na zangu.
“Mwanaharamu mkubwa wewe unakanyaga hayo makochi unasaidia kufua??” nilisikia sauti ya Monica akigomba. Nikasita kufua nikatazama huku na huko, Jonas hayupo. Kule ndani nikazidi kusikia Monica akigomba. Masikio yangu mara yakasikia Jonas akitoa kilio kikali.

Mbiombio nikakimbilia ndani, Jonas alikuwa analia kwa uchungu huku akiwa amejishika shavu. Aliponiona akanikimbili na kunikumbatia huku akiwa analia, aliponikumbatia akawa ameachia lile shavu.

Macho yangu yakaona alama za vidole vya mtu mzima.
Monica alikuwa amemnasa kibao Jonas.
Na hapo nikaisikia sauti ya Jonas akilaumu kitoto toto.
“Mama huyu pigaaaa….” Ilikuwa ni sauti ya kitoto lakini iliyotangaza uchungu. Nikanyanyua macho yangu na kumtazama Monica, nikamkuta akiwa ametingwa katika kufanya lolote alilokuwa akifanya katika luninga.
Mbiombio nikamvamia, yeye na luninga wakaenda chini, nikamweka vyema uso wake, na hapo nikamgeuza kitoweo changu. Nilimpiga haswa!!

Akaja na mdogo wake nikawachanganya wote, nilikuwa na hasira kali kupita nyingine zilizopita.
Nilijua kuwa sihitajiki tena katikia mji ule, nami niliomba mwezi mmoja niweze kuondoka wakanikubalia. Sasa wanamuita Jonas mwanaharamu!!
Gusa pengine usimguse mtoto huyu, nililaaniwa mimi na si Jonas!!

Wakati natoka mlangoni nikakutana na mama Aswile. Sikujali lolote nikaelekea katika chumba changu, nikakusanya nguo zangu huku nikiwa natetemeka, Jonas akiwa mgongoni. Nikasikia chumba kikivamiwa, ni jambo nililolitarajia. Haraka nikageuka nikakutana na mama Aswile. Alikuwa amevimba huku akiwa ameshika mwiko. Taratibu nikamshusha Jonas. Halafu nikahamishia balaa kwa mama mAswile, nilimpiga huku nikimtuhumu kuwa amelaaniwa kwa kuwafanya watoto wake wanichukie bila sababu. Nilihakikisha amenyooka.

Baada ya hapo nikabeba kilicho changu na kuingia katika mitaa ya Tukuyu nikiwa na shilingi elfu tano tu!!
Pesa niliyoipata baada ya mama Aswile kuiangusha akijaribu kukabiliana na mimi!!
Jonas mgongoni, kibegi kidogo mkononi!!
Nikaingia katika mitaa yenye baridi kali. Sina ndugu wala rafiki!!.........USIKOSE SEHEMU YA 21

Hadithi: Usilie Nadia: 19

ILIPOISHIA
Huko chumbani wakati na mimi nabadili nguo nilikuwa nahangaika na utata wa simulizi hiyo yenye maswali mengi!!
 
Sasa Jesca na Nadia wamekutana Dar!! Hivi huu ndo mwisho wa simulizi ama? Lakini haiwezi kuisha maana hali niliyomkuta nayo Nadia Musoma haikuwa ya kawaida hata kidogo sasa alirudi lini Musoma na ni kwanini nilimkuta katika hali ile?? USIKOSE SEHEMU YA 19


SEHEMU YA KUMI NA TISA
Jesca alinieleza kuwa alikuwa na kiasi cha laki saba katika akaunti yake. Hii ilikuwa inatosha sana, ilikuwa ni wakati muafaka wa kumkabili Desmund ili nimpe salamu kutoka katika ile kuzimu ya baharini ambayo nilikuwa na kisha ikazushwa kuwa nimekufa.
Mzee Matata angeongoza mbio hizi za kunieleza ni nanji huyo alitaka kuniua kabla sijaonana na Desmund mume wangu, kila ambaye angenipa jibu hyakika angekuwa amenisaidia sana. Jesca na mwanaye walisinzia lakini mimi nilichelewa sana kulala.

Mwisho nikalala nikiwa na kauli mbiu, nipo hai ili Desmund akome!....mh!! we G wewe yaani ukinogewaga kusikiliza hata kula hunikumbushi au ndo unataka vidonda vya tumbo visimame hapa tuanze kukimbizana hospitali tena” alisema Nadia hapo nami nikakumbuka kuwa kulikuwa na chakula mbele yetu, nikakifunua.

Ewalaa!! Mapaja mawili ya kuku wa kienyeji, wali mweupe na vidikodiko vingine.
Nadia sahani yake na mimi yangu!!!
Kila mtu kwa mwendo wake akaanza kula!!
 Kila mmoja alikuwa na njaa na hakika tulikisosoa chakula kwa wingi, hata Nadia ambaye hawezi kula chakula kingi alijitahidi sana siku hiyo katika kiwango cha kuridhisha. Kama kawaida hakuna aliyesema na mwenzake hadi tuliporidhika, kijana muhudumu akaleta bili nikalipia.
Hapo sasa hapakuwa mahali sahihi pa kuendelea kukaa, nilimwonyesha ishara Nadia nasi tukasimama na kuondoka tukiwa na chupa za maji yetu. Hatukuelekea chumbani, bali siku hii nilimwongoza Nadia hadi katika fukwe za Ziwa Viktoria, jirani na lile jiwe maarufu ama tuseme mwamba maarufu wa Bismark….
Bismark rock!!
Hapakuwa na jua kali hivyo tukaamua kutembea kwa miguu tukapita kona kadha wa kadha hadi tukafika mahali tulipohitaji. Haikuwa mara ya kwanza kwa Nadia kufika eneo lile, lakini wakati wa mwisho kufika hapo labda alikuwa alikuwa katika kipindi kigumu, sasa mimi nilimpeleka pale kwa dhumuni la kupunga upepo na kuendelea kubadilishana mawazo mawili matatu kama yangetokea.
Hapakuwa na watu wengi sana eneo lile hivyo tulipata nafasi ya kujivinjari tuwezavyo kona kadha wa kadha. 
“Mwenzako nayaogopa maji balaa.” Nilimweleza Nadia baada ya kuwaona vijana kadhaa wakiogelea kwa raha kabisa katika maji yale. Nadia alitabasamu kisha akanieleza kuwa yeye ni rafiki wa maji. Nilikumbuka katika mazungumzo alinieleza juu ya namna alivyoweza nkuogelea na kuwakimbia maadui wale waliokuwa wamemteka na kisha kumtumia katika kusafirisha madawa ya kulevya.
“Yaani hapa ningekuwa na nguo za ziada ungeshtukia tu nipo ndani ya maji.” Aliniambia huku akionekana dhahiri kuwa anayatamani yale maji.
“Wewe jifanye kuyazoea maji, maji ni rafiki na ni adui pia…”
“Unajuaje wakati maji ni rafiki na unajuaje kuwa wakati huu ni adui yakiwa yametulia katika namna ile.” Aliniuliza swali ambalo sikulichukulia uzito hata kidogo.
Lakini nilipotaka kulijibu ndipo nikagundua kuwa swali lile ni gumu.
“Kwa kuyatazama huwezi kujua, lakini ukipatwa na kiu na ukayanywa utautambua uzuri wake na ukukizama humo yakakuua utatuachia nafasi tulio hai kuutambua uadui wa maji.” Nilijaribu kumjibu.
“Kwa hiyo huwezi kutambua kwa kuona sivyo.”
“Naam!!” nilimwambia. 
Hapa akafanya tabasamu kidogo.
“Maji ni kama mwanadamu tu, huwezi kuyatambua madhaifu yake mpaka akufanyie jambo fulani.” Akasita kisha akaendelea huku akiyatazama maji. “Wasichana sisi huwa ni wapumbavu sana, yaani wapumbavu wa mwisho kabisa. Si wote lakini hao wapumbavu wanasababisha wote tuonekane sawa. Lakini ‘ishu’ ipo katika kumjua nani mpumbavu na nani si mpumbavu!! Upumbavu huu kwa silimia kubwa huja tukiwa katika mapenzi yaani kama mazezeta vile, basi wanaume wanatufanya watakavyo. Mwandishi unajua Jesca naweza kumuita mjinga ama mpuuzi wa mwisho. Yaani tumehangaika weee tumeshakaa kwenye mstari tunataka kusonga mbele na maisha yetu yeye anafanya mambo ya kijinga na kusababisha turejee tulipotoka.
Mwandishi, tumesafiri vizuri sana yaani wote tukiwa na lengo moja tu kuanza safari yetu ya kimaisha tukitambua kuwa mtoto anatutegemea sisi hivyo kwa ile pesa iliyokuwepo tulitakiwa kufika na kutulia tujue nini tunafanya. Hakika wote tukaunganisha mikono yetu na kuwa kitu kimojha na wazo moja.
Saa saba za usiku tukaingia Mwanza. Nikasimamia jukumu la kutafuta chumba yeye Jesca na mtoto wakabaki stendi wakiningoja. Baada ya dakika kumi na tano nilikuwa nimelipia chumba tayari.
Safari yetu ya kufika Mwanza ikawa imetimia haswa!! Na palipokucha maisha yetu jijini hapo yakaanza rasmi. 
Nilikuwa namuamini samba Jesca na nilimwona ni mwanamke wa shoka lakini kilichokuwa kinanikosesha amani ni hali yake ya kulialia mara kwa mara na kukosa amani.
Moyo wa mtu ni kiza kinene huwezi kujua nini kinajiri humo ndani. Nami sikujua mwenzangu alikuwa anawaza nini, mimi nilijisikia ama kuishi katika nyumba ya kupanga jijini Mwanza hata kama haikuwa na umeme lakini tulikuwa na uhuru lakini mwenzangu alionekana kama maisha yale haridhiki nayo. Nilijiuliza kama alipenda kulawitiwa ili aendelee kuishi maisha bora nyumbani kwa Bryan ama ni kipi kilikuwa kinamnyima amani. Nilitambua kuwa labda kukatisha chuo ghafla nd’o jambo lililoiathiri akili yake nikajipa moyo kuwa labda atakuja kubadilika.,
Kweli ikawa kama nilivyotaraji!! Lakini ilikuwa ghafla sana
Jesca akaanza kupata furaha tena kama kawaida!! Lakini hii furaha ilikuja ghafla sana mwandishi hadi ikanitia mashaka, inakuwaje furaha kama hiyo upesi kiasi hicho? Sikutaka kumuuliza maana swali langu lingemaanisha kuwa mimi nataka awe mpweke kila siku. Wakati huo tulikuwa hatujaanzisha rasmi kitu cha kutuingizia pesa lakini nilikuwa katika michakato ya kufanya biashara ya ushirikiano na mwanamama jirani aliyekuwa anatengeneza supu ya makongoro.
Furaha ya Jesca ikanifanya nikumbuke kila mtu ambaye nimewahi kumuamini na mwisho kunifanya nijute kumuamini. Nikaamua kuchukua tahadhari, na nilijua kama hiyo furaha ina sababu basi sababu ile haitakuwa mbali sana, yaani ikiwa moyoni basi kuiona ni kazi ngumu sana lakini moyo mwingine usiokuwa na siri ni simu ya mkononi. Siku hiyo nikamtegea Jesca alivyoenda kuoga nikaikwapua simu yake bahati nzuri hakuwa ameifunga kwa namba za siri.
Nikakimbilia katika jumbe alizopokea na kutuma, nikakutana na jina baba watoto!!
Ina maana amepata kimwanaume hapa mtaani ama?? Nilijiuliza.
Lakini nikaamua kuzisoma meseji zile ili niweze kupata jibu.
Walikuwa wanajadiliana juu ya safari ya huyo baba watoto kuja jijini Mwanza. Nikaichukua nama upesi nikahifadhi katika simu yangu ambayo nilikuwa nimeinunua siku chache zilizopita.
Meseji nyingine zilitaja jina langu!! Mariam! Nikashangaa ni nani huyo anayenijua mimi.
Meseji ya muhimu kwangu ikawa kwamba yule mtu hakutaka mimi niambiwe kama anakuja eti kisa anataka kunishtua tu!!
“Mimi nilishasamehe mpenzi wangu na ninawapenda sana, kama Mary lazima nimpe zawadi baada ya kumwomba msamaha.” Aliandika huyo baba watoto. 
Nikairejesha simu baada ya kumsikia Jesca anafunga bafu.
Mwandishi, hakuna kitu kibaya katika haya maisha kama kusalitiwa na yule unayempenda, tena ni heri afanye usaliti na uhadithiwe tu lakini sio kushuhudia. Yaani nilihisi kuwa yuyle anayewasiliana na Jesca atakuwa ni Bryan tu, lakini niliamua kuthibitisha nikatafuta simu nyingine nikampigia ili tu kuhakikisha.
Hakika alikuwa ni Bryan yule mwanaharamu aliyetaka kumlawiti Jesca. Yaani leo hii huyu Jesca ambaye niliumia moyo na kuamua kumwepusha na balaa lile kisha tukatoroka na kujiwekea ahadi kuwa hatutakaa tuwasiliane na Br4yan ama familia yake iwapo atakuwa amekufa!
Sasa Jesca anawasiliana na mwanaharamu……
Si nilisema wasichana sisi ni wapumbavu, wapumbavu wa kutupa mwandishi, hivi unamwamini vipi mtu aliyetaka kukulawiti bila huruma, unaanza vipi kumwamini mtu ambaye tulitaka kuupoteza uhai wake?? Kibaya zaidi sasa tulikubaliana kwa pamoja kuwa hatutawasiliana na Bryan lakini katika kuwasiliana naye akaamua kufanya mwenyewe, kwa hiyo mimi sikuwa na maana tena baada ya hayo yote tuliyopanga.
Nililia sana mwandishi. Nililia sana kwa sababu nilikuwa nimesalitiwa, tena nimesalitiwa na mtu ambaye ninamuamini.
Niliamua kujifanya naumwa ilimradi tu Jesca asijue ni kiasi gani amenikwaza na kunitia jeraha!!
Wanawake!! Dhaifu sana sisi, yaani dhaifu hadi kero.
Yaani mapenzi huwa yanakuwa mzigo sana kwetu, nd’o maana wasichana hujikuta wakiwaamini wapenzi wao kuliko wazazi wao wa kuwazaa. Eti kisa tu mpenzi amemuahidi kumuoa. Nayasema haya kwa sababu hata mimi niliwahi kuwa mpumbavu!!
Sikutaka Jesca naye awe mpumbavu, lakini ni kama alikuwa mpumbavu tayari. Ningeanza vipi kumwambia kuwa nilichukua simu yake na kusoma meseji zake. Angenionaje??
“Mariam…kesho nitatoka kidogo mwenzako yaani kuna rafiki yangu nilisoma naye jana kama mchezo nimejaribu anapatikana kwenye simu anakaa huko Airport. Ngoja nikaonane naye dada yangu, maana haya maisha hatutaweza na pesa hiyoo inaisha” Jesca aliniambia wakati tunapata chakula. Nilijisikia hasira sana kwa sababu alikuwa ananidanganya. Kwa nini Jesca ananidanganya wakati mimi nilikuwa muaminifu kwake nikamwokoa asikamatwe na majibu ya mtihani ilhali simjui?? Mbona niliendelea kuwa muaminifu kwake na nikaiweka roho yangu rehani ilimradi nimwokoe asilawitiwe?
Yaani ameshindwa kulipa uaminifu kidogo tu!! Jesca Jesca!!
Sikuweza kuendelea kula tena, nikasingizia kichwa kinaniuma. Nikajitupa katika godoro nikalala.
Nilisinzia nikiwaza jambo moja tu, kama Jesca ameamua kujipeleka katika domo la mamba basi mimi sitakubali hata kidogo Jonas naye atumbukie humo. Alikuwa mtoto mdogo sana kuingia katika kashkash.
 Kesho yake majira ya saa nne asubuhi nikamwona Jesca akimwandaa Jonas, nikamsubiri niisikie kauli yake, majira ya saa tano akataka kutoka na Jonas. Nikamzuia, hakuna kwenda na mtoto huko kwa rafiki.
“Jesca jicho linanichezacheza hautaenda na mtoto kwa kweli kama jicho linanicheza kwa mabaya basi yakusibu wewe mtu mzima utajua kujiokoa lakini Jonas tutakuwa tunamwonea” niliunda uongo.
Alidhani natania lakini kwa mara ya kwanza nikamkunjia sura. Akaogopa akaniaga akiahidi kuwa akirejea nitatabasamu na jicho litaacha kucheza.
“Nakupenda Jesca.” Hilo lilikuwa neno la mwisho kumwambia, akaondoka na sikuwahi kumwambia neno jingine tena.
Alipoondoka na mimi nikaondoka nikiwa na Jonas na akiba ya pesa yote iliyokuwa imebaki. Nikaufunga mlango vyema, nikaweka funguo mahali anapopafahamu Jesca kisha nikaondoka. Nikampeleka Jonas kwa mama ambaye nilikubaliana naye kuungana katika biashara ya makongoro. Uzuri wa Jonas hakuwa akichagua mtu, hakuwa mtoto wa kulialia hovyo labda awe anaumwa.
Nikamwomba mama yule amuhifadhi pale hadi nitakaporejea, akakubali nikamwachia shilingi kadhaa kwa ajili ya dharula kama tu itajitokeza.
Sasa nikarejea kuwa shuhuda wa kitu ambacho kitaenda kutokea, imani yangu ilikuwa ndogo sana kumwamini Bryan niliyempasua na chupa kichwani, lakini ningemsaidia nini Jesca wakati wahenga walisema mkataa pema pabaya panamuita!!
Nilijiweka mahali pazuri nikawa natazama ugeni huo kama utakuja kwa amani.
Muda ulizidi kwenda bila matokeo yoyote.
Saa tisa za alasiri ndipo nikapokea simu kutoka katika namba ya Jesca.
“Mambo dada Mariam, nitachelewa kurudi, si Jonas yupo, niwaletee nini nikija.?” Alijiumauma Jesca, nikajikuta natabasamu kwani nilijua kuwa tayari hakuwa huru tena Jesca. Kitu nilichokuwa nawaza.
Majira ya saa kumi na mbili akanipigia simu akaniuliza kama nipo nyumbani. Kitu ambacho hakikuwa cha kawaida kabisa kwa Jesca, nami nikaendelea kutulia tu. Majira ya saa mbili usiku gari mbili zikafunga breki katika nyumba tuliyokuwa tumepanga. Wakaruka wanaume kwa fujo!! Jicho langu likamuona Jesca, alikuwa amelowa damu, na kisha nikamuona Bryan alikuwa ameiva kwa hasira kali. Nikajilazimisha kutabasamu maana sikuweza na nafsi iliniambia kuwa nitakuwa mjinga kumsaidia mpumbavu!!
Nikatoweka kimyakimya huku nikiwaachja wajinga hao wakitangaza kuwa ‘Mariam popote pale ulipo jitokeze’
Nikaondoka huku nikiumia sana hakika kwa hali aliyokuwanayo Jesca, usiri wake na kuamini mapenzi ya kijinga kulimponza. 
Nilifika nyumbani kwa yule mama majira ya saa nne usiku, nikamchukua Jonas na kuondoka naye. 
Hapo nikakumbuka kuwa nilikuwa nimelaaniwa na huenda ile laana ya mama ilisema kuwa nitaishi kama kivuli sitatulia wala kupata amani, hakuna atakayenipenda hata kidogo licha ya kujipendekeza kwake.
Naam!! Nilikuwa mkimbizi tena.
Nikalala nyumba ya kulala wageni pamoja na Jonas!!
“Jonas, sijui kama utamuona mama yako tena. Nasema sijui kwa sababu anajua mwenyewe ni wapi alipo. Hautakaa utulie tena maana utaandamana na mwenye laana Nadia, hautatabasamu tena kwasababu upo na nyumba ya kilio Nadia, hautakuwa na uhuru kwa sababu upo na mfungwa Nadia. Lakini kikubwa amini kuwa huyu mfungwa atakufa naye atakuacha, lakini hatakufa kizembe kama mmama yako, hatashikika kipuuzi kwa mapenzi na kubwa zaidi akifa atakuacha ukiwa katika mikono ya yeyote yule ambaye hajalaaniwa. Utamuita mama naye atakuita wewe mtoto wake. Sitakuacha Jonas hadi roho yangu itakapouacha mwili!!!” nilizungumza na kitoto kile kilichokuwa kinanitazama tu bila kusema chochote!!
Asubuhi nilikuwa mkiimbizi kuelekea mahali pengine!! Mwanza haikunifaa tena, mropokaji aitwaye Jesca angeweza kunichoma.
Nikazima simu yangu na kusahau kabisa kama niliwahi kuwa na simu!!!”…akasita Nadia akatazama kushoto na kulia.
“Wee G hapa huwa pabaya usiku wanakaba sana mwenzangu na hii afya yangu mgogoro wasije wakaniua bure….” Kauli hii ikanishtua, kweli palikuwa na giza na tulikuwa tumebaki watu wachache sana, tukasimama na kujikongoja tukapata teksi kwa ajili ya kuturudisha hotelini.
Kila mmoja alikuwa kimya!!
 Nilikuwa na swali moja kubwa. Nadia alisema kuwa hatamwacha Jonas hadi yeye afe kwanza, sasa mbona Jonas hayupo na yeye yupo hai?? 
Nini kilitokea na kusababisha haya!!!
Na nini hatima ya Jesca…….

Hadithi: Usilie Nadia. 17 na 18


 ILIPOISHIA
Hilo likawa neno lake la mwisho kwa kiingereza akaanza kuzungumza kiarabu cha ndani kabisa. Alinivuta lakini sikutaka kumfuata. Niliendelea kung’ang’ania vyuma nilivyokuwa nimeshikilia. Lakini nilijua tu ni mfa maji haishi kutapatapa…….” Akasita kisha akaendelea, “Yaani nimesema maji nd’o nakumbuka tumenunua maji na hadi sasa hatujanywa!! Duh yasije yakawa ya moto tena.” Alisema Nadia kisha akachukua maji nami nikatwaa yangu, hakika makoo yalikuwa yamekaua haswaa!!USIKOSE SEHEMU YA 17

SEHEMU YA KUMI NA SABA

“Katika maisha wanadamu huwa ni wagumu sana kuamini kuwa Mungu yupo hasahasa wakati wa shida ama tatizo kubwa. Mungu hukumbukwa wakati wa raha tu. Utawasikia maharusi wakimshukuru Mungu kwa kuwafanikishia jambo hilo walilolingoja kwa muda mrefu lakini ni nadra sana kuwasikia wafiwa wakimshukuru Mungu waziwazi kwa kumtwaa mojawapo kati ya wapendwa wao!! Wanadamu sisi watu wa ajabu sana!! Nawakumbuka rafiki zangu wengi tu walivyofeli masomo yao hawakumwambia Mungu asante kama walivyofanya baada ya kufaulu!!” Nadia alinieleza maneno yale baada ya kuwa amekunywa nusu chupa ya yale maji. Nami nikatikisa kichwa kumuunga mkono.


“Hata mimi ni mmojawao, mmoja kati ya wasiomkumbuka na kumuamini Mungu wawapo katika shida ngumu. Badala yake kutarajia miujiza ya kidunia. Maana katika giza lile ambalo nilikuwa kisha yule muuaji akanikamata miguu sikutarajia lolote linaweza kufanyika kwa muujiza wa Mungu na badala yake niliendelea kuamini kuwa ni mimi pekee wa kuweza kuiokoa nafsi yangu. 

Niliendelea kutapatapa huku na kule nikiling’ang’ania chuma ambalo lilibaki kuwa muhimili wangu mkuu, na yeye aliendelea kunivuta huku akizidi kuweka viapo vikali vya kuniua kwa kunikatakata. Labda ulikuwa wakati wa kujikabidhi kwa Mungu lakini ningeanza vipi kuamini kuwa Mungu alikuwa upande wangu wakati kila baya linalotokea aliwashindia maadui zangu na akiniacha mimi katika majeraha? Nikajiaminisha kuwa yule hakuwa Mungu wangu bali Mungu wa maadui zangu.

Naam!! Huenda aliisikia sauti yangu, labda alingoja niwe katika wakati mgumu kama ule nd’o aweze kujionyesha kwangu!! Lile chuma ambalo nilikuwa nalitegemea sasa lilianza kulegea kutokana na kuvutwa sana na yule mzee wa kiarabu tuliyezoea kumuita masta. Hapo sasa nikakata tamaa, nikataka kujiachia lakini nafsi ikagoma kukata tamaa nikaendelea kushikilia japo nilikuwa nazidi kulisikia likisogea na mimi.

Mara likafyatuka!!

Nilichoweza kukisikia ni yowe la hofu kutoka kwa yule mwarabu, na baada ya hapo maji yalitusomba kwa nguvu mno na kisha kuanza kusdafiri nasi, ni hapo ndipo nikatambua kuwa chuma niliyokuwa nimeshikilia ilikuwa ni ufunguo wa aidha tanki la maji ama chochote kile. Lakini ajabu ni uwingi wa maji yale, nikajishukuru kwa kutokuwa mvivu kujifunza kuogelea enzi hizo nikitumikia uvuvi nyumbani kwao Desmund, nilikata maji kwa mwendo mkali, hofu ikiwa imetanda hasahasa lile giza nene, giza likiwa limetawala. Nilijigonga huku na kule lakini sikubadili azma yangu ya kutapatapa kama nitakufa nife nikiwa najaribu!! Baada ya kuogelea kwa dakika kadhaa hatimaye niliweza kuona mwanga. Hapakuwa na giza tena, niliangaza kushoto na kulia baada ya kunyanyua kichwa changu, nikawaona watu kwa mbali, hivyo nikatambua kuwa sikuwa mbali sana kutoka katika ufukwe. Hofu nyingine ilikuwa juu ya nchi ambayo ningeweza kuwepo na watu wa pale ufukweni, isijekuwa ni walewakle waliokuwa wametuteka wakanikamata tena. Nikazama tena majini na kuanza kupiga mbizi. Na nilipoibuka tena ndipo nilipokutana na maajabu makubwa ambayo sikuyatarajia hata kidogo!!

Nikaona PANTONI…..lilelile la Kigamboni!!

Kwa hiyo pale tulikuwa Dar esa salaam!!

Nilistaajabu huku nikiendelea kukata maji, sikujua hata ni wapi nilitokea hadi kufika pale nilipokuwa, lakini nilitilia mashaka maggorofa kadhaa yaliyokuwa kandokando na bahari ya hindi.  Nikaufikia ufukwe, mavazi yangu yakiwa tepetepe, ubize wa watu jijini Dar es salaam ukanisaidia sana, hakuna aliyekuwa na habari na mwenzake katika ufukwe ule. Nilijituliza huku nikitafakari ni kipi kinafuata katika maisha yangu baada ya Mungu kuniepusha na mauti yale?

Hakika ni Mungu tu, maana kwa uweza wangu hakuna ambalo ningeweza kufanya.

Jua likapiga na upepo ukapuliza mavazi yangu yakapata hali ya ukavu kiasi!!

Na akili nayo ikachangamka na kutambua kuwa kuna uwezekano mkubwa sana wale watu watakuwa wakinitafuta. Na iwapo wakinikamata wataniua maana kuna siri tayari nilikuwa nimezijua, utumwa katika nchi huru, tena utumwa wenye adhabu nzito ndani yake. Uuzaji wa madawa ya kulevya!!

Nikasimama wima, walau nilikuwa katika jiji ambalo nilikuwa nalifahamu, lakini ni jiji ambalo bila kuwa na pesa hauna maana ya kuwa hapo nadhani unalijua vyema, nami sikuwa na nauli wala mtu ninayemfahamu pale. Nikiwa wima nikajiuliza niende wapi, mwisho nikaamua kuelekea Vijibweni, ni huku tuliwahi kuishi na familia yangu kabla sijaamua kuasi na kuungana na Desmund katika mahusiano ya mashaka, mateso na karaha tupu huku yakiichafua historia yangu jumla. Nilipiga hatua moja baada ya nyingine, kutoka kivukoni hadi Kibada si karibu hata kidogo nililazimika kutembea sana. Hatimaye nikaifikia ile nyumba ambayo zamani nilikuwa nikikohoa kidogo tu nasikilizwa, nyumba ambayo mlinzi alikuwa akiniogopa na kuniheshimu zaidi ya mbwa mkali. Nyumba ambayo familia yenye upendo na amani iliishi humo. Nikainama chini na kujitazama, sikuwa na viatu na nguo niliyovaa ilikuwa imechakaa, nikajifikiria jinsi kichwa changu kisichokuwa na nywele nyingi jinsi kisivyotamanisha hata kukitazama. Kwa unyonge kabisa nikapiga hatua tena nikalifikia geti.

Nikajipa moyo kuwa labda habari za kwenda Saudi Arabia ni uongo mtupu familia yangu itakuwepo.

Labda hata habari za mama kufariki ni uongo vilevile alikuwa hai na wote walikuwa ndani, labda hata mlinzi aitwaye Hamduni nitamkuta na ataniheshimu tena.

Wakati naduwaa mara geti lilifunguliwa ghafla, akatoka mlinzi akiwa na bunduki aina ya gobole mkononi. Alikuwa ameikunja sura yake akinitazama mimi.

“Wewe ni nani ana unataka nini hapa?” alinikoromea! Nilikuwa katika mshtuko bado nikabaki kumwangalia badala ya kumjibu, akanirukia na kunikwida na kisha kurudia swali lilelile

“Naitwa Mariam!” nilimjibu.

“Sijakuuliza jina kichaa wewe, unafanya nini hapa muda huu?” aliniuliza kwa jazba. Kabla sijajibu akaendelea, “Hapa haturuhusu hayo mambo yenu ya kuombaomba sijui” alisema lakini mara akanikazia macho katika kifua changu!! Nami nikajitazama, nilikuwa natokwa damu.

“Umekuwaje binti!!” sasa aliniuliza kwa upole.

“Naitwa Mariam, wazazi wangu wanaishi katika nyumba hii”

“Wazazi wako?...maskini madawa ya kulevya kila siku wanakataza maskini. Binti mzuri kama huyu na yeye yamemwathiri looh!! Kijana taifa la kesho huu usemi ufutwe sasa.” Alilalamika peke yake, nikajua anahisi mimi nimeathirika na madawa.

“Mzee Barghash ni baba yangu.” Niliongezea.

“Binti….njia ile pale waweza kwenda zako mbali na hapa.”

“Babu sijachanganyikiwa, situmii madawa ya kulevya, nina akili zangu timamu, niulize lolote nami nitakujibu!! Tafadhali nisaidie nionane nao.”

“Binti leo tarehe ngapi mwezi wa ngapi? Na ni mwaka gani huu achana na tarehe kwanza.” Aliniuliza kama kunipima akili. Hakika alikuwa amenipata vilivyo, sikujua hata huo ulikuwa mwaka gani na sikujua hata nimekaa kule mafichoni kwa muda gani. Lakini nikajitahidi niweze kujibu ili aweze kuniamini.

Nikajiaminisha kuwa huenda hata mwaka mmoja haujaisha tangu nitupwe kule. Nikaamua kukadiria kuwa ulipita mwaka

“Mwaka 2010…”

“Yesu wangu weee!! Binti toka na upotee mbele yangu mara moja nasema.”

“Babu nipe nafasi ya mwisho. Nisikilize tafadhali.”

Wakati anataka kunitishia bunduki mara mtu mmoja akatokea getini, na kumshangaa yule mzee.

“Kababu huyu ni nani? Bona chafu chafu tu navaa uchi hapa” sauti ya mama wa kihindi. Ikakoroma huku akinitazama kwa sekunde moja huku sekunde nyingine akimtazama mlinzi. Ile hali ya kuhangaika kuzungumza Kiswahili ikanipa upenyo wa kujaribu bahati yangu ya kuuthibitishia umma kuwa sikuwa kichaa.

“Excuse me madame! Can I talk to you..pleasee!!” nilimsihi kwa lugha ya kiingereza, hapo akashtuka na kisha kuniuliza kwa kiingereza huku akiwa na wasiwasi na mlinzi naye akinishangaa.

“Wewe ni nani.’ Akaniuliza, nikajieleza vyema ubin wangu.

“Ooooh!! Baba yako alituuzia nyumba hii miaka mingi sasa hadi leo 2010 ni muda sana. Kumbe wewe ni mtoto wake, nini kimekutokea?” alinieleza na ni hapo nikatambua kuwa nimekaa kule sirini kwa miaka miwili tangu 2009 na huo mwaka ulikuwa 2011. Nikabaki kinywa wazi. Hapakuwa na jipya nikajaribu kuulizia kuhusu majirani, mama yule hakuwa akimfahamu hata mmoja.

Kisha akaamuru geti likafungwa!!

Nikatakiwa kupotea eneo lile.

Nikatii lakini nikamwomba mlinzi kidogo anisikilize.

“Jizungushe pita baada ya dakika kumi apotee.” Aliniambia, nikajiondokea. Nikapita huku na kule kama nitakuta wale majirani wa miaka hiyo lakini haikuwa hivyo, palikuwa na watu wagenmi tu!!

Baada ya dakika kumi nikarejea. Nikamwomba mlinzi aniazime simu yake nipige. Aliniangalia kwa mashaka nami nikagundua hofu yake.

“Nikutajie namba unipigie hizo namba tafadhali nakuomba.” Nilimsihi, akanielewa.

Nikajaribu kuvuta kumbukumbu, nikataja na kungoja majibu.

Simu ikaanza kuita!! Mara ya kwanza haikupokelewa!!

Mara ya pili ikapokelewa na mwanaume, jambo ambalo sikulitarajia.

Mlinzi akaniamini akanipa simu nizungumze huku akiiweka sawa bunduki yake, bila shaka kitisho nisikimbie na simu yake.

“Samahani, naomba kuongea na nani huyu? Naomba kuongea na mwenye simu kakangu.” Nilijikuta nasema.

“Mimi ndiye mwenye simu aisee.” Alinijibu kwa jeuri.

Nikaishiwa usemi lakini mara nikamsikia akisema maneno chinichini na hatimaye akaanza kuongea msichana.

“Halo! Samahani nikumbushe jina lako tafadhali.”

“Yaani wewe unapiga na hujui unayempigia.”

“Samahani wewe ni Jesca.”

“Kwani wewe unampigia nani?” aliniuliza na mlinzi naye alikunja sura akionyesha kujutia pesa ilivyokuwa inateketea katika simu yake.

“Nampigia Jesca tafadhali.” Nilisihi.

“Ni mimi nini shida na nani mwenzangu?”

“Jesca mimi Mariam, mimi Nadia Jesca!!! Jesca kama ni wewe kweli tambua kuwa nipo katika shida kubwa.”

“Nadiaaaa!!! Nadiaaaa!!!” alihamanika huko alipokuwa.

Simu nayo ikakatika!!

Mlinzi akaanza kulaumu, mara simu ikaita kwa namba mpya tofauti na ya Jesca, mlinzi akapokea.

Alikuwa Jesca.

“Nadia nilijua haujafa, nilijua wamekusingizia Nadia, nilijua ni njama….nililia Nadia, nililia sana lakini sikuwa tayari kusema ulazwe pema peponi, sikuwa tayari Nadia. Sauti yako ipo hai Nadia, nakupenda Nadia wangu, upo wapi Nadia.” Aliongea kwa hisia kali Jesca, machozi yakaanza kunibubujika.

“Nipo kama sipo, nipo kama mzimu, sina nguo za kuvaa, sina chakula, sina mahali pa kuishi. Ni afadhali ningekuwa katika kambi za wakimbizi. Jesca labda ni bora ningekuwa nimekufa, lakini ninayopitia ni zaidi ya mahangaiko. Jesca nakupenda sana na namba yako haikufutika katika kichwa changu kamwe. Nilikwambia ni wewe pekee ndugu yangu katika dunia hii. “

“Mtanimalizia chaji yangu!!” alilalamika mlinzi.

‘Jesca upo wapi kwani.”

“Nipo mlimani mpenzi. Nipo huku chuoni.”

“Jesca jamani!!! Hadi umefika chuo, mimi nipo huku Kibada, kama nilivyokwambia sina hali.”

“Kibada ni wapi??”

“Kigamboni…” nilimjibu nikamsikia akimuuliza yule mvulana aliyepokera simu mara ya kwanza.

“Baby Kibada unapajua”..kisha baada ya dakika kadhaa akaniambia, “tunakuja huko muda si mrefu eti utungojee Kigamboni huohuo upande wa pili..”

“Jesca natamani ungepewa macho, unione nilivyovimba miguu, upewe na tumbo langu uisikie hii njaa kali inayioishi humu, Jesca sitaweza kufika Kigamboni. Nitafia njiani!!” nilimnweleza. Nikamsikia akilia kwa kwikwi kutoka upande wa pili.

“Basi tunakuja hadi huko!! Usijali.” Aliniambia.

“Sawa mtatumia namba hii babu ataniambia.” Nilihitimisha.



Kisha nikazungumza na babu akakubaliana na mimi, nikaahidi kuwa wakifika nitampa chochote kitu atie mfukoni. Hapo nikamteka.

Nikaondoka pale na kujiweka mbali kidogo, nilipokaa chini nikakumbuka kumshukuru Mungu wangu!!! Alikuwa akinionyesha miujiza.



Baada ya masaa mawili na nusu hatimaye nikaona gari likisimama kwa mbali, babu akanipungia mkono. Nikakimbia mbio kwenda alipokuwa.

“Wapo ndani ya gari ile, usisahau chochote kitu!!”

Hapo hapo nikatimua mbio, mara mlango wa gari ukafunguliwa haraka akatoka binti akiwa amevaa kisasa sana, sketi fupi mno na viatu virefu. Akaweka urembo wake kando akavua viatu na kuanza kutimua mbio.

Harufu ya upendo ikasafiri na kuzifikia pua zangu, macho yanayomaanisha yanachotazama yakanieleza kuwa yule alikuwa Jesca. Naam! Hatimaye tukakutana ana kwa ana tukarukiana na kukumbatiana kwa nguvu, hiyo haikutosha Jesca akajisahau kuwa mimi nina njaa akanirukia tukaanguka chini lakini furaha haikupotea hata kidogo!!

Jesca alikuwa analia na machozi yake yaliangukia katika mabega yangu!!

Alikuwa amekuwa mdada mkubwa tena wa kisasa!!



Baada ya kusalimiana nikamkumbuka babu, Jesca akanipatia noti mbili nyekundu nikampelekea, mzee hakuamini lakini nadhani alitambua kuwa wema wake na imani yake kwangu vilikuwa vikubwa sana!!



“Bryan….anaitwa Mariam ni dada yangu. Na…Mariam huyu anaitwa Bryan ni mchumba wangu. Mengi tutayafahamu mbele kwa mbele.” Alitambulisha Jesca. Kisha nikapakizwa ndani ya gari tukaondoka!!

Wanasema kuwa baada ya dhiki ni faraja lakini kwa Nadia mimi kila baada ya dhiki ilikuwa inakuja dhiki nyingine inayofanana na faraja kisha inanisulubu. Hata hapa nilipokuwa sikutaka kujidanganya kuwa nimefika katika kikomo cha mateso!! Lakini walau nilikuwa katika mikono ya Jesca, na hapo niliweza tena ku….” Nadia akanitazama kisha akatabasamu!! Nikaelewa alikuwa anamaanisha nini kuikatisha ile kauli.

“Hee!! Yaani kumbe unanisikiliza tu hata kusema Nadia twende kula muda umefika aa mwanaume mbaya wewe dah!! Mwone!! Mi nina njaa mwenzako sio siri, ile kapuchino yote imamemalizika tumboni…”

“Niwapigie simu walete huku ama..”

“Hamna hawa wakileta huku huwa wanapunja sana. Twende hukohuko yaani wakinipunja tu naenda jikoni mwenyewe kujipakulia.” Alitania Nadia, tukajikuta tunacheka wote.

“Haya basi nipishe nibadili nguo mwenzako.’ Aliniomba, nami nikatoka nje ya chumba chake na kwenda katika chumba changu. 



Huko chumbani wakati na mimi nabadili nguo nilikuwa nahangaika na utata wa simulizi hiyo yenye maswali mengi!!

Sasa Jesca na Nadia wamekutana Dar!! Hivi huu ndo mwisho wa simulizi ama? Lakini haiwezi kuisha maana hali niliyomkuta nayo Nadia Musoma haikuwa ya kawaida hata kidogo sasa alirudi lini Musoma na ni kwanini nilimkuta katika hali ile??

INAPOENDELA  SEHEMU YA 18
“Katika maisha wanadamu huwa ni wagumu sana kuamini kuwa Mungu yupo hasahasa wakati wa shida ama tatizo kubwa. Mungu hukumbukwa wakati wa raha tu. Utawasikia maharusi wakimshukuru Mungu kwa kuwafanikishia jambo hilo walilolingoja kwa muda mrefu lakini ni nadra sana kuwasikia wafiwa wakimshukuru Mungu waziwazi kwa kumtwaa mojawapo kati ya wapendwa wao!! Wanadamu sisi watu wa ajabu sana!! 

Nawakumbuka rafiki zangu wengi tu walivyofeli masomo yao hawakumwambia Mungu asante kama walivyofanya baada ya kufaulu!!” Nadia alinieleza maneno yale baada ya kuwa amekunywa nusu chupa ya yale maji. Nami nikatikisa kichwa kumuunga mkono.


 
“Hata mimi ni mmojawao, mmoja kati ya wasiomkumbuka na kumuamini Mungu wawapo katika shida ngumu. Badala yake kutarajia miujiza ya kidunia. Maana katika giza lile ambalo nilikuwa kisha yule muuaji akanikamata miguu sikutarajia lolote linaweza kufanyika kwa muujiza wa Mungu na badala yake niliendelea kuamini kuwa ni mimi pekee wa kuweza kuiokoa nafsi yangu. 

Niliendelea kutapatapa huku na kule nikiling’ang’ania chuma ambalo lilibaki kuwa muhimili wangu mkuu, na yeye aliendelea kunivuta huku akizidi kuweka viapo vikali vya kuniua kwa kunikatakata. Labda ulikuwa wakati wa kujikabidhi kwa Mungu lakini ningeanza vipi kuamini kuwa Mungu alikuwa upande wangu wakati kila baya linalotokea aliwashindia maadui zangu na akiniacha mimi katika majeraha? Nikajiaminisha kuwa yule hakuwa Mungu wangu bali Mungu wa maadui zangu. 

 
Naam!! Huenda aliisikia sauti yangu, labda alingoja niwe katika wakati mgumu kama ule nd’o aweze kujionyesha kwangu!! Lile chuma ambalo nilikuwa nalitegemea sasa lilianza kulegea kutokana na kuvutwa sana na yule mzee wa kiarabu tuliyezoea kumuita masta. Hapo sasa nikakata tamaa, nikataka kujiachia lakini nafsi ikagoma kukata tamaa nikaendelea kushikilia japo nilikuwa nazidi kulisikia likisogea na mimi.
 
Mara likafyatuka!! 

 
Nilichoweza kukisikia ni yowe la hofu kutoka kwa yule mwarabu, na baada ya hapo maji yalitusomba kwa nguvu mno na kisha kuanza kusdafiri nasi, ni hapo ndipo nikatambua kuwa chuma niliyokuwa nimeshikilia ilikuwa ni ufunguo wa aidha tanki la maji ama chochote kile. Lakini ajabu ni uwingi wa maji yale, nikajishukuru kwa kutokuwa mvivu kujifunza kuogelea enzi hizo nikitumikia uvuvi nyumbani kwao Desmund, nilikata maji kwa mwendo mkali, hofu ikiwa imetanda hasahasa lile giza nene, giza likiwa limetawala. Nilijigonga huku na kule lakini sikubadili azma yangu ya kutapatapa kama nitakufa nife nikiwa najaribu!! Baada ya kuogelea kwa dakika kadhaa hatimaye niliweza kuona mwanga. Hapakuwa na giza tena, niliangaza kushoto na kulia baada ya kunyanyua kichwa changu, nikawaona watu kwa mbali, hivyo nikatambua kuwa sikuwa mbali sana kutoka katika ufukwe. Hofu nyingine ilikuwa juu ya nchi ambayo ningeweza kuwepo na watu wa pale ufukweni, isijekuwa ni walewakle waliokuwa wametuteka wakanikamata tena. Nikazama tena majini na kuanza kupiga mbizi. Na nilipoibuka tena ndipo nilipokutana na maajabu makubwa ambayo sikuyatarajia hata kidogo!!
 
Nikaona PANTONI…..lilelile la Kigamboni!!
 
Kwa hiyo pale tulikuwa Dar esa salaam!!

 
Nilistaajabu huku nikiendelea kukata maji, sikujua hata ni wapi nilitokea hadi kufika pale nilipokuwa, lakini nilitilia mashaka maggorofa kadhaa yaliyokuwa kandokando na bahari ya hindi.  Nikaufikia ufukwe, mavazi yangu yakiwa tepetepe, ubize wa watu jijini Dar es salaam ukanisaidia sana, hakuna aliyekuwa na habari na mwenzake katika ufukwe ule. Nilijituliza huku nikitafakari ni kipi kinafuata katika maisha yangu baada ya Mungu kuniepusha na mauti yale?
 
Hakika ni Mungu tu, maana kwa uweza wangu hakuna ambalo ningeweza kufanya.
 

Jua likapiga na upepo ukapuliza mavazi yangu yakapata hali ya ukavu kiasi!!
 
Na akili nayo ikachangamka na kutambua kuwa kuna uwezekano mkubwa sana wale watu watakuwa wakinitafuta. Na iwapo wakinikamata wataniua maana kuna siri tayari nilikuwa nimezijua, utumwa katika nchi huru, tena utumwa wenye adhabu nzito ndani yake. Uuzaji wa madawa ya kulevya!!
 
Nikasimama wima, walau nilikuwa katika jiji ambalo nilikuwa nalifahamu, lakini ni jiji ambalo bila kuwa na pesa hauna maana ya kuwa hapo nadhani unalijua vyema, nami sikuwa na nauli wala mtu ninayemfahamu pale. Nikiwa wima nikajiuliza niende wapi, mwisho nikaamua kuelekea Vijibweni, ni huku tuliwahi kuishi na familia yangu kabla sijaamua kuasi na kuungana na Desmund katika mahusiano ya mashaka, mateso na karaha tupu huku yakiichafua historia yangu jumla. Nilipiga hatua moja baada ya nyingine, kutoka kivukoni hadi Kibada si karibu hata kidogo nililazimika kutembea sana. Hatimaye nikaifikia ile nyumba ambayo zamani nilikuwa nikikohoa kidogo tu nasikilizwa, nyumba ambayo mlinzi alikuwa akiniogopa na kuniheshimu zaidi ya mbwa mkali. Nyumba ambayo familia yenye upendo na amani iliishi humo. Nikainama chini na kujitazama, sikuwa na viatu na nguo niliyovaa ilikuwa imechakaa, nikajifikiria jinsi kichwa changu kisichokuwa na nywele nyingi jinsi kisivyotamanisha hata kukitazama. Kwa unyonge kabisa nikapiga hatua tena nikalifikia geti.

 
Nikajipa moyo kuwa labda habari za kwenda Saudi Arabia ni uongo mtupu familia yangu itakuwepo.
 
Labda hata habari za mama kufariki ni uongo vilevile alikuwa hai na wote walikuwa ndani, labda hata mlinzi aitwaye Hamduni nitamkuta na ataniheshimu tena.
 
Wakati naduwaa mara geti lilifunguliwa ghafla, akatoka mlinzi akiwa na bunduki aina ya gobole mkononi. Alikuwa ameikunja sura yake akinitazama mimi.
 
“Wewe ni nani ana unataka nini hapa?” alinikoromea! Nilikuwa katika mshtuko bado nikabaki kumwangalia badala ya kumjibu, akanirukia na kunikwida na kisha kurudia swali lilelile
 
“Naitwa Mariam!” nilimjibu.
 
“Sijakuuliza jina kichaa wewe, unafanya nini hapa muda huu?” aliniuliza kwa jazba. Kabla sijajibu akaendelea, “Hapa haturuhusu hayo mambo yenu ya kuombaomba sijui” alisema lakini mara akanikazia macho katika kifua changu!! Nami nikajitazama, nilikuwa natokwa damu.
 
“Umekuwaje binti!!” sasa aliniuliza kwa upole.
 
“Naitwa Mariam, wazazi wangu wanaishi katika nyumba hii”
 
“Wazazi wako?...maskini madawa ya kulevya kila siku wanakataza maskini. Binti mzuri kama huyu na yeye yamemwathiri looh!! Kijana taifa la kesho huu usemi ufutwe sasa.” Alilalamika peke yake, nikajua anahisi mimi nimeathirika na madawa.
 
“Mzee Barghash ni baba yangu.” Niliongezea.
 
“Binti….njia ile pale waweza kwenda zako mbali na hapa.”
 
“Babu sijachanganyikiwa, situmii madawa ya kulevya, nina akili zangu timamu, niulize lolote nami nitakujibu!! Tafadhali nisaidie nionane nao.”
 
“Binti leo tarehe ngapi mwezi wa ngapi? Na ni mwaka gani huu achana na tarehe kwanza.” Aliniuliza kama kunipima akili. Hakika alikuwa amenipata vilivyo, sikujua hata huo ulikuwa mwaka gani na sikujua hata nimekaa kule mafichoni kwa muda gani. Lakini nikajitahidi niweze kujibu ili aweze kuniamini.
 
Nikajiaminisha kuwa huenda hata mwaka mmoja haujaisha tangu nitupwe kule. Nikaamua kukadiria kuwa ulipita mwaka
 
“Mwaka 2010…”
 
“Yesu wangu weee!! Binti toka na upotee mbele yangu mara moja nasema.”
 
“Babu nipe nafasi ya mwisho. Nisikilize tafadhali.”
 
Wakati anataka kunitishia bunduki mara mtu mmoja akatokea getini, na kumshangaa yule mzee.
 
“Kababu huyu ni nani? Bona chafu chafu tu navaa uchi hapa” sauti ya mama wa kihindi. Ikakoroma huku akinitazama kwa sekunde moja huku sekunde nyingine akimtazama mlinzi. Ile hali ya kuhangaika kuzungumza Kiswahili ikanipa upenyo wa kujaribu bahati yangu ya kuuthibitishia umma kuwa sikuwa kichaa.
 
“Excuse me madame! Can I talk to you..pleasee!!” nilimsihi kwa lugha ya kiingereza, hapo akashtuka na kisha kuniuliza kwa kiingereza huku akiwa na wasiwasi na mlinzi naye akinishangaa.
 
“Wewe ni nani.’ Akaniuliza, nikajieleza vyema ubin wangu.
 
“Ooooh!! Baba yako alituuzia nyumba hii miaka mingi sasa hadi leo 2010 ni muda sana. Kumbe wewe ni mtoto wake, nini kimekutokea?” alinieleza na ni hapo nikatambua kuwa nimekaa kule sirini kwa miaka miwili tangu 2009 na huo mwaka ulikuwa 2011. Nikabaki kinywa wazi. Hapakuwa na jipya nikajaribu kuulizia kuhusu majirani, mama yule hakuwa akimfahamu hata mmoja.
 
Kisha akaamuru geti likafungwa!!
 
Nikatakiwa kupotea eneo lile.
 
Nikatii lakini nikamwomba mlinzi kidogo anisikilize.
 
“Jizungushe pita baada ya dakika kumi apotee.” Aliniambia, nikajiondokea. Nikapita huku na kule kama nitakuta wale majirani wa miaka hiyo lakini haikuwa hivyo, palikuwa na watu wagenmi tu!!
 
Baada ya dakika kumi nikarejea. Nikamwomba mlinzi aniazime simu yake nipige. Aliniangalia kwa mashaka nami nikagundua hofu yake.
 
“Nikutajie namba unipigie hizo namba tafadhali nakuomba.” Nilimsihi, akanielewa.
 
Nikajaribu kuvuta kumbukumbu, nikataja na kungoja majibu.
 
Simu ikaanza kuita!! Mara ya kwanza haikupokelewa!!
 
Mara ya pili ikapokelewa na mwanaume, jambo ambalo sikulitarajia.
 
Mlinzi akaniamini akanipa simu nizungumze huku akiiweka sawa bunduki yake, bila shaka kitisho nisikimbie na simu yake.
 
“Samahani, naomba kuongea na nani huyu? Naomba kuongea na mwenye simu kakangu.” Nilijikuta nasema.
 
“Mimi ndiye mwenye simu aisee.” Alinijibu kwa jeuri.
 
Nikaishiwa usemi lakini mara nikamsikia akisema maneno chinichini na hatimaye akaanza kuongea msichana.
 
“Halo! Samahani nikumbushe jina lako tafadhali.”
 
“Yaani wewe unapiga na hujui unayempigia.”
 
“Samahani wewe ni Jesca.”
 
“Kwani wewe unampigia nani?” aliniuliza na mlinzi naye alikunja sura akionyesha kujutia pesa ilivyokuwa inateketea katika simu yake.
 
“Nampigia Jesca tafadhali.” Nilisihi.
 
“Ni mimi nini shida na nani mwenzangu?”
 
“Jesca mimi Mariam, mimi Nadia Jesca!!! Jesca kama ni wewe kweli tambua kuwa nipo katika shida kubwa.”
 
“Nadiaaaa!!! Nadiaaaa!!!” alihamanika huko alipokuwa.
 
Simu nayo ikakatika!!
 
Mlinzi akaanza kulaumu, mara simu ikaita kwa namba mpya tofauti na ya Jesca, mlinzi akapokea.
 
Alikuwa Jesca.
 
“Nadia nilijua haujafa, nilijua wamekusingizia Nadia, nilijua ni njama….nililia Nadia, nililia sana lakini sikuwa tayari kusema ulazwe pema peponi, sikuwa tayari Nadia. Sauti yako ipo hai Nadia, nakupenda Nadia wangu, upo wapi Nadia.” Aliongea kwa hisia kali Jesca, machozi yakaanza kunibubujika.
 
“Nipo kama sipo, nipo kama mzimu, sina nguo za kuvaa, sina chakula, sina mahali pa kuishi. Ni afadhali ningekuwa katika kambi za wakimbizi. Jesca labda ni bora ningekuwa nimekufa, lakini ninayopitia ni zaidi ya mahangaiko. Jesca nakupenda sana na namba yako haikufutika katika kichwa changu kamwe. Nilikwambia ni wewe pekee ndugu yangu katika dunia hii. “
 
“Mtanimalizia chaji yangu!!” alilalamika mlinzi.
 
‘Jesca upo wapi kwani.”
 
“Nipo mlimani mpenzi. Nipo huku chuoni.”
 
“Jesca jamani!!! Hadi umefika chuo, mimi nipo huku Kibada, kama nilivyokwambia sina hali.”
 
“Kibada ni wapi??”
 
“Kigamboni…” nilimjibu nikamsikia akimuuliza yule mvulana aliyepokera simu mara ya kwanza.
 
“Baby Kibada unapajua”..kisha baada ya dakika kadhaa akaniambia, “tunakuja huko muda si mrefu eti utungojee Kigamboni huohuo upande wa pili..”
 
“Jesca natamani ungepewa macho, unione nilivyovimba miguu, upewe na tumbo langu uisikie hii njaa kali inayioishi humu, Jesca sitaweza kufika Kigamboni. Nitafia njiani!!” nilimnweleza. Nikamsikia akilia kwa kwikwi kutoka upande wa pili.
 
“Basi tunakuja hadi huko!! Usijali.” Aliniambia.
 
“Sawa mtatumia namba hii babu ataniambia.” Nilihitimisha.
 

 
Kisha nikazungumza na babu akakubaliana na mimi, nikaahidi kuwa wakifika nitampa chochote kitu atie mfukoni. Hapo nikamteka.
 
Nikaondoka pale na kujiweka mbali kidogo, nilipokaa chini nikakumbuka kumshukuru Mungu wangu!!! Alikuwa akinionyesha miujiza.
 

 
Baada ya masaa mawili na nusu hatimaye nikaona gari likisimama kwa mbali, babu akanipungia mkono. Nikakimbia mbio kwenda alipokuwa.
 
“Wapo ndani ya gari ile, usisahau chochote kitu!!”
 
Hapo hapo nikatimua mbio, mara mlango wa gari ukafunguliwa haraka akatoka binti akiwa amevaa kisasa sana, sketi fupi mno na viatu virefu. Akaweka urembo wake kando akavua viatu na kuanza kutimua mbio.
 
Harufu ya upendo ikasafiri na kuzifikia pua zangu, macho yanayomaanisha yanachotazama yakanieleza kuwa yule alikuwa Jesca. Naam! Hatimaye tukakutana ana kwa ana tukarukiana na kukumbatiana kwa nguvu, hiyo haikutosha Jesca akajisahau kuwa mimi nina njaa akanirukia tukaanguka chini lakini furaha haikupotea hata kidogo!!
 
Jesca alikuwa analia na machozi yake yaliangukia katika mabega yangu!!
 
Alikuwa amekuwa mdada mkubwa tena wa kisasa!!
 

 
Baada ya kusalimiana nikamkumbuka babu, Jesca akanipatia noti mbili nyekundu nikampelekea, mzee hakuamini lakini nadhani alitambua kuwa wema wake na imani yake kwangu vilikuwa vikubwa sana!!
 

 
“Bryan….anaitwa Mariam ni dada yangu. Na…Mariam huyu anaitwa Bryan ni mchumba wangu. Mengi tutayafahamu mbele kwa mbele.” Alitambulisha Jesca. Kisha nikapakizwa ndani ya gari tukaondoka!!
 
Wanasema kuwa baada ya dhiki ni faraja lakini kwa Nadia mimi kila baada ya dhiki ilikuwa inakuja dhiki nyingine inayofanana na faraja kisha inanisulubu. Hata hapa nilipokuwa sikutaka kujidanganya kuwa nimefika katika kikomo cha mateso!! Lakini walau nilikuwa katika mikono ya Jesca, na hapo niliweza tena ku….” Nadia akanitazama kisha akatabasamu!! Nikaelewa alikuwa anamaanisha nini kuikatisha ile kauli.
 
“Hee!! Yaani kumbe unanisikiliza tu hata kusema Nadia twende kula muda umefika aa mwanaume mbaya wewe dah!! Mwone!! Mi nina njaa mwenzako sio siri, ile kapuchino yote imamemalizika tumboni…”
 
“Niwapigie simu walete huku ama..”
 
“Hamna hawa wakileta huku huwa wanapunja sana. Twende hukohuko yaani wakinipunja tu naenda jikoni mwenyewe kujipakulia.” Alitania Nadia, tukajikuta tunacheka wote.
 
“Haya basi nipishe nibadili nguo mwenzako.’ Aliniomba, nami nikatoka nje ya chumba chake na kwenda katika chumba changu. 
 

 
Huko chumbani wakati na mimi nabadili nguo nilikuwa nahangaika na utata wa simulizi hiyo yenye maswali mengi!!
 
Sasa Jesca na Nadia wamekutana Dar!! Hivi huu ndo mwisho wa simulizi ama? Lakini haiwezi kuisha maana hali niliyomkuta nayo Nadia Musoma haikuwa ya kawaida hata kidogo sasa alirudi lini Musoma na ni kwanini nilimkuta katika hali ile?? USIKOSE SEHEMU YA 19
 
 
Blogger Templates