Social Icons

Friday, 9 December 2016

Mashambulizi dhidi ya IS yashika kasi

Vikosi vya wapiganaji wa kikurdi wa kundi la Pershmega walioko nchini Iraqi leo wameushambulia mji unaoshikiliwa na kundi la kigaidi la Dola la Kiislamu, IS, ulioko KaskaziniMashariki mwa mji wa Mosul, Bashiqa.

Irak Mossul Gogjali, Häuserkampf Irakische Armee (picture-alliance/AP Photo/M. Drobnjakovic) )

Mashambulizi hayo ni sehemu ya mkakati wa kuwafurusha wapiganaji wa kundi hilo la Dola la Kiislamu nje ya mji huo, wakati ambapo majeshi ya Iraqi nayo yakianzisha mashambulizi ndani ya mji na wapiganaji wa jihadi katika eneo la jirani la Mashariki mwa Mosul. 

Kundi la kwanza la kikosi cha wapiganaji 2000 wa Pershmega liliingia kwene eneo la Bashiqa, wengi wao wakiwa na magari yaliyosheheni silaha na wengine wakitembea kwa miguu, baada ya mji huo kushambuliwa kwa mizinga.
  
Wapiganaji wa kundi la IS, wametaka kupunguza mashambulizi katika mji wa Mosul, ambao ni ngome pekee wanayoishikilia kwenye mapigano ambayo leo hii yanaingia wiki ya nne, huku kukiwa na mashambulizi ya mabomu ya kujitoa muhanga yaliyotegwa kwenye magari. Makamanda wa Iraqi wanasema kulikuwa na wapiganaji 100, waliokuwa mstari wa mbele katika eneo la Mashariki na wengine 140 eneo la Kusini.

Wapiganaji hao wa Kikurdi wameendelea kukabiliana na wapiganaji wa IS, wakati wakiendelea kusonga mbele kutoka maeneo mawili tofauti wakiusogelea mji wa Bashiqa, ulioko Mashariki mwa Mosul unaoshikiliwa na kundi hilo la kigaidi. Mashambulizi yaliyofanywa asubuhi hii ni sehemu ya mpango wa kuwafurusha IS kutoka Mosul, mji ambao ni wa pili kwa ukubwa nchini Iraqi.

Syrien SDF PK Sturm auf Rakka (Getty Images/AFP/D. Souleiman)

Msemaji wa vikosi vya usalama vya Syria, Jihan Sheikh Ahmed akitangaza kuanza kwa mashambulizi ya kuuchukua mji wa Raqa, unaoshikiliwa na kundi la Dola la Kiislamu.

Bashiqa inayoaminika kukaliwa na wapiganaji wengi wa IS iko Kilomita 13 Kaskazini Mashariki mwa Mosul. Wapiganaji hao wa IS bado wanashikilia eneo kubwa lililoko Kaskazini, Kusini na Magharibi mwa Mosul, na wameendelea kusogeleea maeneo yanaokaliwa na raia wengi ili kuwatumia kama ngao ya vita.

Hata hivyo kutoka vikosi vya pershmega, Brigedier General Iskander Khalil Ghardi amesema, taarifa za kiintelijensia zinaeleza kuwa hakuna wakaazi wengi waliosalia Bashiqa, na hivyo vikosi vyake vitazidi kusonge mbele.

Katika hatua nyingine, majeshi ya Syria yanayoungwa mkono na Marekani yameanzisha mashambulizi mapya ya kuurejesha mji wa Raqqa, ambao pia ni ngome ya wapiganaji wa IS nchini Syria. Mashambulizi hayo pacha, ya Mosul na Raqqa yanataraji kuondoa kabisa mfumo wa kimadhehebu uliotangazwa na kiongozi wa kundi la Dola la Kiilsamu, Abu Bakr al-Baghdad.

Baghadadi aliwaambia wafuasi wake kwamba hakuna kurudi nyuma katika vita hivyo na maadaui zao. 

Na huko Kusini mwa Mosul, majeshi ya usalama yamesema yameurejesha mji wa Hamman al Alil kutoka kwa wapiganaji wa kundi la Dola la Kiislamu, ambao kulingana na maelezo yao, wapiganaji hao walikuwa wamewahifadhi raia wengi watakaowatumia kama ngome ya vita, huku wakiwatanguliza raia wengine mbele ya wapiganaji waliokuwa wakielekea Mosul ili kukabiliana na mashambulizi ya anga. 

Na eneo la Kusini mwa Mosul, taarifa za kijeshi zinasema Kikosi cha 16 cha jeshi lake kimefanikiwa kukirejesha kijiji cha Bawiza na kuingia kwenye eneo jingine, Sada, lililopo kwenye mipaka, Kaskazini mwa Mosul, hatua inayoongeza ugumu dhidi ya vikosi vya wapiganaji vya IS. 

Chanzo. Dw.de

Mashambulizi yanafanyika kwa msaada wa Marekani

Vikosi vinavyoungwa mkono na Marekani vimeongeza mashambulizi dhidi ya ngome muhimu zinazodhibitiwa na wapiganaji wa kundi linalojiita Dola la Kiislamu-IS, nchini Syria na Iraq.

Irak Kampf um Mossul gegen den IS (picture-alliance/Anadolu Agency/H. Baban)

Wakisaidiwa na mashambulizi ya anga ya muungano wa majeshi yanayoongozwa na Marekani, vikosi vya Iraq vimezidi kusonga mbele kuingia Mosul, ngome kuu ya IS, huku muungano wa wapiganaji wa Kikurdi wakielekea Raqqa, Syria, mji ambao ni ngome kuu ya wapiganaji hao wa jihadi.

Shirika linalofuatilia haki za binaadamu nchini Syria lenye makao yake mjini London, Uingereza, limesema vikosi vya anga jana usiku, vimeshambulia kijiji cha Al-Heisha kinachodhibitiwa na IS, ambacho kiko umbali wa kilomita 40 kaskazini mwa Iraq.

Mkurugenzi wa shirika hilo, Rami Abdul Rahman, amesema mashambulizi ya Raqqa yamesababisha mauaji ya raia 20, huku wanawake wanane na watoto wawili wakiwa miongoni mwa waliouawa na wengine 32 wamejeruhiwa. Hata hivyo, msemaji wa vikosi vinavyopigania demokrasia nchini Syria-SDF, ambavyo vinaungwa mkono na Marekani, Jinah Sheikh Ahmed, amekanusha kutokea kwa mauaji hayo ya raia na kwamba madai yoyote kama hayo yanatolewa na IS.

Syrien SDF PK Sturm auf Rakka (Getty Images/AFP/D. Souleiman)

WAnajeshi wa vikosi vya SDF

Msemaji wa muungano wa majeshi unaoongozwa na Marekani, Kanali John Dorrian amesema inaonekana kuwa mashambulizi yamefanyika kwenye eneo hilo. Amesema baada ya kufanyika tathmini ya awali, muungano huo umethibitisha kwamba ulifanya mashambulizi kwenye eneo ambalo limeelezwa. Hata hivyo, panahitajika taarifa zaidi zitakazoonyesha hitimisho kwamba wahanga wa mashambulizi hayo ni raia. Kwa mujibu wa vikosi vya SDF, kiasi ya familia 200 zimekikimbia kijiji cha Al-Heisha.

Mashambulizi yalianza Jumamosi

Siku ya Jumamosi vikosi vya usalama vya Iraq, vilianzisha operesheni yenye lengo la kuwafurumusha wapiganaji wa IS, kutoka kwenye mji wa Mosul. Taher Farhan, afisa polisi wa shirikisho la Iraq amesema ushindi utapatikana hivi karibuni.

''Tunakaribia kushinda, tuna matumaini kwamba umebaki muda kidogo tu hadi tutakapokamilisha kazi ya kuikomboa Mosul. Sasa tuko Hammam al-Alil, tunashukuru Mungu tumeweza kulisafisha eneo hili na kama mnavyoona familia zimerudi hapa,'' alisema Farhan.

Syrien Rakka U.S. Soldaten (Reuters/R. Said)

Wanajeshi wa Marekani wanaosaidia mashambulizi ya Iraq na Syria

Wakati huo huo, Shirika la kimataifa la haki za binaadamu, Amnesty International limesema vikosi vya serikali vya Iraq vinawatesa na kuwaua wanakijiji wa kusini mwa Mosul. Hiyo ni ripoti ya kwanza kutolewa kuhusu ukiukwaji wa haki za binaadamu tangu kuanza kwa mashambulizi ya kuukomboa mji wa Mosul kutoka kwa IS.

Shirika hilo limesema wahanga ni pamoja na watu sita waliogunduliwa mwezi uliopita kwenye wilaya ndogo za Shura na Qayyara, ambazo vikosi vya usalama vinashuku vina mafungamano na kundi la IS ambalo liliutwaa mji huo mwaka 2014. Hata hivyo, msemaji wa jeshi la polisi la Iraq na wizara ya mambo ya ndani, hakuweza kupatikana mara moja kuzungumzia madai hayo.

Chanzo. Dw.de


Watu 120 wauawa kwenye mashambulio ya angani nchini Irak

Mashambulio hayo yametokea katika mji wa Qaim unaoshikiliwa na wapiganaji wa IS nchini Irak. Watu wengine 170 wamejeruhiwa katika mashambulizi hayo katika eneo la magharibi mwa Irak karibu na mpaka wa Syria.

Kampf um Mossul (picture-alliance/dpa/A. Jalil)

Spika wa bunge la Irak, Salim al-Jabouri amesema kwamba serikali ya Irak inapaswa kubeba dhamana ya makosa hayo yaliyotokea na vile vile ianzishe uchunguzi utakaobaini ukweli wa mauaji hayo, na  wakati huo huo ameitaka serikali iwahakikishie raia kuwa tukio kama hilo linalo walenga raia moja kwa moja halitatokea tena.

Mashambulio hayo yalilenga katika eneo la soko kwenye mji huo wa Qaim ulioko Magharibi mwa nchi, takriban kilomita 500 kutoka mji mkuu wa Baghdad. Mbunge Fares al Fares ameeleza kwamba ndege za Irak zilifanya mashambulio hayo ingawa hakutoa maelezo zaidi. Hali kadhalika, hadi sasa serikali haijatoa tamko lolote kuhusiana na mashamabulizi hayo. Mnamo miezi ya hivi karibuni vikosi vya Irak vinavyoungwa mkono na Marekani vimekuwa vikiendeleza mashambulio dhidi ya wapiganaji wa IS ambao waliyanyakua maeneo mengi katika mashambulizi yenye kasi kubwa mnamo mwaka 2014.

Duru za hospitali pamoja na baadhi ya wabunge zinaelezea juu ya kutokea mashambulio matatu ya angani katika mji huo wa Qaim.  Msemaji wa kikosi kinachoongozwa na Marekani kinachoshirikiana na majeshi ya Irak katika mapambano dhidi ya IS amekanusha kuwa wamehusika na mashambulio hayo ya angani ambayo kitengo cha habari cha IS kinaelekeza lawama kwa vikosi vya kijeshi vya serikali.

Salim al-Jubouri neuer Parlamentspräsident von Irak Archiv 2010 (picture alliance/AP Photo)

Salim al-Jabouri Spika wa bunge la Irak

Salim al-Jabouri mwanasiasa mashuhuri wa Kisunni na wa ngazi ya juu katika siasa za Irak, amesema mashambulio hayo yalilenga kimakusudi katika maeneo ya raia kwa mfano maduka ndio maana watu wengi wameuwawa na wengine wengi wamejeruhiwa. Kwa kiwango kikubwa nchi ya Irak inaongozwa na wanasiasa wa Kishia, mji wa Qaim na eneo lote la mkoa wa magharibi ni sehemu ambayo ina Wassuni wengi na pia bado inashikiliwa na kundi la IS.  Mashambulio hayo yametokea wakati ambapo majeshi ya serikali ya Irak yanaendeleza kampeni yake ya wiki saba yenye lengo la kuwaangamiza wapiganaji wa IS ambao pia wameuteka mji wa Mosul ulio takriban kilomita 280 kaskazini mashariki mwa mji huo wa Qaim.

Katika siku za hivi karibuni wapiganaji wa IS wameshindwa vibaya katika mapigano katika mji wa Mosul nchini Irak na pia katika mji wa Aleppo nchini Syria.

Chanzo. Dw.de

Syria na Ukraine kutawala mkutano wa OSCE

Wakati Ujerumani inakamilisha muhula wa mwaka mmoja kama mwenyekiti wa Shirika la Usalama na Ushirikiano barani Ulaya-OSCE, Waziri wake wa Mambo ya Nje, Frank-Walter Steinmeier, ameitaka Urusi kushirikiana kikamilifu.

Hamburg OSZE-Treffen Steinmeier Rede (picture-alliance/dpa/C. Charisius)

Wito huo ameutoa jana usiku kabla ya kuanza kwa mkutano wa siku mbili wa OSCE mjini Hamburg, Ujerumani, ambao unatarajiwa kutawaliwa na ajenda kuhusu Syria na Ukraine. Wakati wa mkutano wake na mwenzake wa Urusi, Sergei Lavrov, siku moja kabla ya mkutano huo unaoanza leo, Steinmeier amesema Urusi inahitaji kusaidia kupunguza mivutano inayoongezeka barani Ulaya.

Ameitaka Urusi kutekeleza haraka mpango wa kusitisha mapigano nchini Syria, ili kuruhusu misaada ya kibinaadamu kuingia nchini humo. Steinmeier amemtaka Lavrov kushinikiza kuwepo suluhisho la kisiasa katika mzozo wa Syria ulioanza mwaka 2011.

Karibu mawaziri 50 wa mambo ya nje pamoja na maafisa wa ngazi za juu wanakutana leo mjini Hamburg, katika Baraza la 23 la Mawaziri wa OSCE, huku ulinzi ukiwa umeimarishwa kwenye mji huo.

Deutschland Vorbereitung auf das OSZE-Treffen in Hamburg (picture alliance /dpa/ B. Marks)

Polisi akilinda doria Hamburg

Polisi wamesema zaidi ya maafisa wa usalama 10,000 wamepelekwa mjini humo ili kuhakikisha usalama katika mkutano huo wa ngazi ya juu.

Urusi na mzozo wa Crimea

Kuhusu suala la Ukraine, Steinmeier ameikosoa Urusi kwa kuhusika katika mzozo wa mashariki mwa nchi hiyo, pamoja na kuitwaa Rasi ya Crimea mwaka 2014, baada ya rais wa Ukraine aliyekuwa akiungwa mkono na Urusi, Viktor Yanukovych kuondolewa madarakani. Aidha, ameitaka Urusi ihakikishe amani inarejea barani Ulaya. Amesema wanaamini kuwa baada ya kumalizika kwa Vita Baridi, suala la vita na amani linapaswa liwe limemalizika kabisa barani Ulaya, lakini bara hilo limekuwa katika migogoro ya mara kwa mara.

''Suala la vita na amani limerejea tena barani Ulaya, baada ya Urusi kujitwalia Crimea na mpaka sasa mchakato wa amani haujazaa matunda, licha ya kuwepo juhudi kadhaa za kumaliza mzozo huo. Na kwa sababu ya hilo, ni muhimu mataifa yote ya Ulaya yakaungana pamoja kwa ajili ya mazungumzo ya ana kwa ana yatakayosaidia kumaliza mizozo barani Ulaya na nje ya bara hilo, na sio tu kutoa matamko kupitia umma,'' amesema Steinmeier.

Italien Außenminister Russland & USA Treffen in Rom Sergej Lawrovw & John Kerry (Reuters/G. Borgia)

Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergei Lavrov (Kushoto) na mwenzake wa Marekani, John Kerry (Kulia) wakiwa Hamburg

Muda mchache kabla ya kukutana na Steinmeier, Lavrov alikutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry na kuzungumzia mikakati ya kumaliza mapigano kwenye mji wa Aleppo, Syria. Kerry amewaambia waandishi wa habari mjini Hamburg, kwamba wamebadilishana mawazo kuhusu Aleppo na wanadhamiria kushirikiana ili kukomesha mapigano mjini humo.

Lavrov amesema amelikubali na kuthibitisha kuliunga mkono pendekezo la Marekani la ''Disemba 2'' linalotaka waasi kujiondoa kabisa kutoka mashariki mwa Aleppo. Hata hivyo, kuna uwezekano kwamba Urusi isifikie makubaliano yoyote hadi Rais Mteule wa Marekani, Donald Trump atakapoingia madarakani. Umoja wa Mataifa unakadiria kuwa watu 300,000 bado wamezingirwa ndani ya mji wa Aleppo.

Chanzo. Dw.de

 
 
Blogger Templates