Baada ya kupata maelezo hayo wazazi wa mwanafunzi huyu walichukua hatua ya kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi cha Kiwira. Polisi walichukua hatua ya kumtafuta diwani Mwakalibule na kumuweka chini ya ulinzi wakati upelelezi wa tukio hili ukiendelea. Mtuhumiwa kwa sasa anashikiliwa katika kituo cha polisi cha Wilaya ya Rungwe mjini Tukuyu.
Mpaka mwandishi wetu anatoka katika kituo cha polisi mjini Tukuyu mtoto wa shule alikuwa amepelekwa hospitali ya Wilaya ya Rungwe 'Makandana' kwa uchunguzi zaidi wa kitaalamu.
Kituo cha Polisi Tukuyu mahali ambako Diwani wa Kata ya Kiwira Lawland Mwakalibule anashikiliwa na jeshi la Polisi kwa tuhuma za kufanya mapenzi na mtoto wa shule ya Sekondari Kiwira.
Diwani wa Kata ya Kiwira Lawland Mwakalibule akiwa chini ya ulinzi wa Polisi katika kituo kikuu cha Polisi mjini Tukuyu.
Picha zote na Basahama blog.
No comments:
Post a Comment