Social Icons

Thursday, 17 October 2013

DR. MARY MWANJELWA: CCM TUNAJIMALIZA SISI WENYEWE

Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa akiongea kwenye kongamano la kumuenzi Mwalimu Nyerere lililoandaliwa na wasomi wa Vyuo Vikuu vilivyoko Mkoani Mbeya.



         Dr. Mary Mwanjelwa akiendelea kuwapa nasaha vijana  katika ukumbi wa Mtenda

           Dr. Mary Mwanjelwa akikabidhi kadi kwa wananchama wapya wa UVCCM


                    Wanachama wapya wa UVCCM  wakila kiapo cha uaminifu 

                                           Vijana wa UVCCM mjini Mbeya


MBUNGE wa viti maalumu mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, amesema baadhi ya wanachama wa chama hicho wanakiangusha chama wao wenyewe kutokana na chuki na kutokumaliza makundi ya uchaguzi.

Hayo aliyaeleza wakati wa kongamano la kumuenzi Baba wa Taifa  Mwalimu Nyerere lililoandaliwa na wasomi wa vyuo vikuu mkoani Mbeya, katika ukumbi wa Mtenda ambako yeye alikuwa mgeni rasmi.
' Tumekuwa mabubu, hatusemi mambo ambayo serikali inafanya, unafiki umezidi ndani ya chama na wengine wanachukia wakielezwa ukweli wakati chama chetu kinajipambanua kuwa ni muhimu kukosoana. Alisema Dr. Mary Mwanjelwa.

                                                     Picha na Kalulunga blog.







No comments:

 
 
Blogger Templates