Social Icons

Tuesday 22 April 2014

CHADEMA WAENDELEA KUPUKUTIKA

Katibu Mwenezi wa CHADEMA Jiji la Mbeya Lucas Mwampiki amejiuzuru

Katibu Mwenezi wa Chama cha Demokrasia Jiji la Mbeya Lucas Mwampiki

Katibu Mwenezi wa Chama cha Demokrasia Jiji la Mbeya Lucas Mwampiki amejiuzuru wadhifa huo kuanzia Aprili mwaka huu kutokana na mkanganyiko wa uongozi ndani ya chama hicho.

Mwapiki amesema amechoshwa na marumbano ya mara kwa mara na meza kuu ndani ya chama hicho katika ngazi ya wilaya hivyo kudhoofisha juhudi zake za kukijenga chama hicho.

Aidha Mwampiki amesema viongozi wa chama hicho wamekuwa na marumbano ya mara kwa mara hivyo yeye kama kiongozi hayupo tayari kuona mambo yanavurugika katika chama hicho.

Hata hivyo katika uamuzi aliouchukua Lucas Mwapiki amesema kuwa yeye atabakia kuwa mwanachama wa chama hicho na Diwani wa Kata ya Mwakibete Jijini Mbeya.

Amewataka wanachama wamuelewe hivyo ameona yeye akae pembeni badala ya kuwa na muda mwingi wa kujadili migogoro ambayo haina tija na kuleta mkanganyiko kwa wanachama.


Na Ezekiel Kamanga
Mbeya yetu

No comments:

 
 
Blogger Templates