Social Icons

Thursday 8 February 2018

Tarehe sita muhimu zinazoeleza kwanini Zuma anakabiliwa na shinikizo

Rais Jacob ZumaHaki miliki ya pichaEPA

Rais wa Afrika kusini Jacob Zuma anakabiliwa na shinikizo ajiuzulu wakati wanachama wakuu wa chama chake walio na uwezo wa kumtimua wakitafakari hatua yao inayofuata.

Ameuhudumu kama rais kwa takribana thuluthi moja ya utawala wa nchi hiyo baada ya ubaguzi wa rangi, lakini uongozi wake umegubikwa kwa kashfa.

Kwa hivyo ni nini kilichotokea kutufikisha hapa tulipo? Haya ni matukio makuu.

14 June 2005: Afutwa kazi

Kwa wakati huu Zuma alikuwa naibu rais aliye na umaarufu na mkakamavu kwa miaka sita - lakini aliipoteza kazi yake baada ya kutuhumiwa katika kesi ya rushwa.

Kwa muda mrefu ameonakana kama mrithi wa rais aliyekuwepo - Thabo Mbeki.

Akiwa kijana alijiunga katika vita vya kupinga ubaguzi wa rangi katika chama cha African National Congress (ANC) na jeshi lake la chini chini kabla ya kufungwa huko Robben Island na Nelson Mandela.

Thabo Mbeki Jacob Zuma - Juni 1999Haki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGES
Image captionBwana Mbeki (kushoto) na Zuma baada ya hotuba yake ya kwanza bungeni mnamo 1999

Mnamo 1997, alikuwa naibu rais wa chama tawala ANC, na baadaye alitajwa kuwa naibu wa rais nchini Afrika kusini mnamo 1999.

Baadaye aligubikwa katika mzozo kuhusu biashara ya silaha yenye thamani ya $ bilioni 5 mnamo 2009 iliyohusisha kampuni kadhaa za Ulaya.

Mshauri wa fedha wa Zuma, Schabir Shaik, alipatikana na hatia ya rushwa na udanganyifu.

Katika kesi hiyo, Zuma alituhumiwa katika kesi hiyo ya rushwa na wakati amekana daima tuhuma hizo, aliipoteza kazi yake. Alishtakiwa mnamo 2007.

6 Aprili 2009: Wiki mbili

Jitihada za rais Zuma kuwania urais zilikuwa zimefika kikomo wakati waendesha mashtaka walipoamua kutomshtaki dhidi ya biashara hizo ya silaha.

Mwendesha mashtaka mkuu nchini amesema ushaihdi uliotokana na kunaswa mawasiliano ya simu unaonyesha kuwa mashtaka hayo mnamo 2007 yalichochewa kisiasa.

Upinzani mkuu waliishutumu hatua hiyo na kuitaja kuwa "utumiaji mbaya" wa jukumu la mwendesha mashtaka. Hatahivyo Zuma, ambaye wakatihuo alikuwa rais wa ANC aliishia kushinda urais wa nchi wiki mbili baadaye.

31 Machi 2016: Kidimbwi maridadi, lakini nani aliyekilipia?

NkandlaHaki miliki ya pichaGOOGLE
Image captionPicha ya satelaiti mnamo 2013 zinaonyesha ukarabati wa mkaazi ya Zuma

Mahakama ya juu ya Afrika ksuini imeamua kuwa Zuma alikiuka katiba wakati aliposhindwa kuilipa serikali pesa alizotumia kwa ujenzi wa makaazi yake binfasi.

Shirika la kupambana na rushwa lilifichua kwamba ametumia $milioni 23 katika makaazi yake Nkandla katika jimbo la KwaZulu-Natal na kujenga kidimbwi cha kuogolea na na chumba cha kutizama filamu. Baadaye alizilipa pesa hizo.

Kwa mara nyengine akakabiliwa na shinikizo la kujiuzulu. Na kwa mara nyengine hakujiuzulu.

Jacob ZumaHaki miliki ya pichaAFP / GETTY IMAGES

13 Oktoba 2017: Mashtaka yarudi upya

Mahakama ya rufaa ya juu zaidi Afrika kusini iliamua kuwa ni lazima Zuma ajibu mashtaka 18 ya rushwa, udanganyifu, na biashara haramu ya fedha yanayohusiana na biashara ya 1999 ya silaha.

Yote haya yalitokana na kesi iliyowasilishwa na chama cha upinzani Democratic Alliance katika mahakama ya Pretoria kikitaka rais akabiliwe na mashtaka. Zuma alikata rufaa, lakini alishindwa.

13 Desemba 2017: Hukumu mbili, siku mbaya

Kwanza mahakama ya Pretoria ilimuamuru Zuma aunde jopo wanasheria la uchunguzi dhidi ya tuhuma za rushwa dhidi yake na washirika wake , ambalo hatimaye aliliunda mnamo Januari.

Uchunguzi huo ni mojawapo ya mapendekezo yaliowasilishwa na tume ya kupambana na rushwa kuistisha maafisa wa serikali kuingilia kati katika kesi hiyo, hatua ambayo Zuma alijaribu kuipinga.

Jaji Dunstan Mlambo alitaja jitihada hizo za uma kujaribukuzuia hukumu kama ushauri m'baya na ukiukaji wa mfumo wa sheria.

Kisha, kwa kando, jaji mmoja aliamua kuwa rais alikiuka mfumo wa sheria kwa kujaribu kuzuia ripotikuhusu rushwa.

Takwimu zinazojitokeza katika tuhuma dhidi ya Zuma ni familia tajiri ya Kihindi kwa jina GUpta wanaotuhumiwa kutumia urafiki wao na rais kushawishi uteuzi wa mawaziri bungeni na kujipatia kandarasi za serikali.

Familia ya Gupta na Bwana Zuma wamekana makosa yoyote lakini tuhuma hizo bado zinaglipo.

18 Disemba 2017: Mrithi wa Zuma ateuliwa

Cyril Ramaphosa is one of South Africa's wealthiesHaki miliki ya pichaREUTERS

Katika ushindani wa kumrithi Zuma baada ya miaka 10 kama kiongozi wa ANC,Cyril Ramaphosa naibu rais wa Afrika kusini aliibuka mshindi. Alirithi uwenyekiti wa chama hicho katia wakati ambapo kinapoteza umaarufu chini ya utawala wa Zuma.

Alifanya kampeni kama mgombe aliye dhidi ya Zuma, na aliahidi kukabiliana na rushwa. Ushindi wake ulimueka katika nafasi ya nguvu dhidi ya rais, na kumfanya mgombea mkuu anayeweza kumrithi.

Chanzo. bbc

No comments:

 
 
Blogger Templates