Social Icons

Saturday 12 October 2013

SABABU ZA MWALIMU KUNG'ATUKA KATIKA UONGOZI.


Kwa mujibu wa wajuzi wa mambo Nyerere aliweka wazi dhamira yake hiyo mwishoni ya miaka ya sabini, ambapo alibainisha wazi kuwa angestaafu mwaka 1980.

Lakini kabla ya kuikamilisha dhamira yake, nchi ya Tanzania ikaingia kwenye vita kati yake na Uganda.

Vita hiyo ilikuwa kati ya mwaka 1978 na 79. Mwalimu Nyerere akiwa Amiri Jeshi Mkuu aliongoza vita hiyo hadi pale Tanzania ilipoibuka mshindi na kuikomboa ardhi yao, ambayo Uganda ilikuwa na mpango wa kuitaifisha.

Kutokana na ukweli kuwa hali ya nchi haikuwa nzuri kiuchumi na hata kiusalama, hivyo akaombwa aendelee na uongozi kwa miaka mitano zaidi.

Na hapo ndipo alipoendelea na uongozi hadi Novemba 7, 1985, alipoamua kung’atuka rasmi katika nafasi zake zote za uongozi ndani ya Chama na Serikali.

Tukio la kung’atuka kwake kutoka katika nafasi zake hizo limekuwa likitafsiriwa kwa mitazamo tofauti tofauti, licha ya ukweli kuwa hiyo haikuwa mara ya kwanza kwake kufikia uamuzi huo.

Awali alishawahi kuachia ngazi katika madaraka yake ya Uwaziri Mkuu mwaka 1962, ili aende akaimarishe chama chake cha TANU.

Mwalimu Nyerere alipoeleza nia yake ya kung’atuka madarakani kama rais na baadaye kama mwenyekiti wa CCM, wananchi wengi sana walionyesha hofu kubwa, na hata baadhi yao walijaribu kumzuia asiondoke madarakani.

Licha ya ukweli huo lakini bado Mwalimu Nyerere alikuwa na sababu zake, zilizomsukuma hadi kufikia uamuzi wake huo.

Je, ungependa kufahamu sababu hizo?

Sababu kuu iliyomfanya baba huyo wa Taifa la Tanzania ang’atuke madarakani, ni pale tu alipoona amekwisha ijenga misingi muhimu na imara.

Misingi hiyo ni pamoja na umoja, amani, upendo, haki, usawa demokrasia uongozi wa nchi na maenedeleo katika nyanja za elimu, uchumi na siasa.

Chanzo:- Mwananchi.

No comments:

 
 
Blogger Templates