Social Icons

Sunday 18 March 2018

WATUMISHI WA AFYA WAASWA KUJIEPUSHA VITENDO VYA RUSHWA SEHEMU ZAO ZA KAZI

NA WAMJW-DAR ES SALAAM


WATUMISHI wa sekta ya Afya nchini wametakiwa kujiepusha na vitendo vya kutaka rushwa kutoka kwa wananchi wanapokuwa sehemu zao za kazi ili kuendana na maadili ya utumishi wa Umma. 

Hayo yamezungumzwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo kilichofanyika leo jijini Dar es salaam ili kujadili mustakabari wa utoaji huduma za Afya nchini. 

“Marufuku Watumishi wa sekta ya afya nchini kujiingiza kwenye vitendo vya rushwa na kama wapo naomba waache mara moja kwani atakayebainika anajihusisha na rushwa sheria itafuata mkondo wake mara moja” alisema Waziri Ummy. Aidha Waziri Ummy amesema kuwa watumishi wa sekta ya afya hasa katika sehemu ya kutolea huduma za afya wanatakiwa kuwa na lugha nzuri kwa wananchi pindi wanapotoa huduma sehemu zao za kazi. 
aziri Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akifungua Mkutano Wa Balaza la Wafanyakazi Wa Wizara ya Afya mapema leo Jijini Dar es salaam.
Mganga Mkuu Wa Serikali Prof. Muhammad Bakari Kambi akimkaribisha mgeni rasmi Waziri Wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu(hayupo kwenye picha)
Mkurugenzi Wa Mafunzo na Rasilimali watu Dkt.Otilie Gowelle wakwanza kulia akifuatilia kwa makini maagizo ya Waziri Wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Afya uliofanyika jijini Dar es salaam.
eza kuu ikiongozwa na Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu na mganga Mkuu wa Serikali Prof. Kambi wakati wakiimba wimbo wa kuhamasisha umoja na mshikamano kwa Wafanyakazi, pindi wakifanya mkutano wa Baraza la Wafanyakazi, Wakwanza ni Katibu wa Baraza hilo Mary Ntira na wa mwisho ni Afisa Elimu kazi na mratibu wa Jinsia taifa TUGHE Bw. Nsubisi Mwasandende
Watumishi wa Wizara ya Afya wakiongozwa na Mkurugenzi wa Tiba Dkt. Dorothy Gwajima wapili kutoka kulia.
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu katikati waliokaa akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa Baraza la wafanyakazi kutoka Wizara ya Afya mara baada ya kikao cha Baraza hilo kilichofanyika Leo jijini Dar es salaam.


Chanzo. Michuzi blog

No comments:

 
 
Blogger Templates