Social Icons

Wednesday, 10 September 2014

HADITHI: Missed call ya shemeji -9


Nawewe unayaweza mama najuta kumfahamu mdogo wako kabla yako, wewe ndiye ulipaswa uwe mke wangu, unipikie, unifulie, uniogeshe na unifanyie mambo mazuri kama haya kila ninapohitaji. Beka alimwambia shemejiye, wakachela
 “Mimi naona  hujaamua tu kufanya hivyo…hata leo ukitaka kumuacha yule chakubimbi wako unaweza…tena ukimuacha nitafurahi sana,” shemeji yake alimwambia Beka.
SASA JIONEZE MWENYEWE…

“Mimi naweza kumfanyia mizengwe mpaka akimbie halafu uchukue nafasi yake tule nanasi kwa nafasi na si kwa kujibanabana!” Beka alimwambia shemeji.

Baada ya kutoa kauli hiyo, shemejiye alikenua meno yote thelathini na mbili nje, akamkumbatia Beka, akambusu midomoni, mume huyo wa mdogo wake akachaji tena, akampa mambo.

Walipomaliza kufurahishana, waliingia bafuni wakaogeshana, wakavaa nguo ndipo Beka akamshauri shemejiye huyo abaki pale kwa muda ili yeye atangulie nyumbani.

Kufuatia shemejiye huyo kufurahishwa na penzi tamu la mume wa mdogo wake, hakuwa na neno alimruhusu kiroho safi, walibusiana na Beka akashika njia kuelekea kwake.

Alipofika alijifanya kushtuka kumkuta mkewe akiwa amejikunyata nje, akamuuliza kulikoni?
“Kila nikikuambia dada yangu hajatulia ndiyo maana kaachwa na mumewe unakuwa upande wake, sasa kaondoka hapa nyumbani bila kuaga mbaya zaidi kaenda kwenye michepuko yake na funguo,” mke wa Beka alimwambia mumewe.

“Inamaana umetafuta kila mahali hujaziona?” Beka alimuuliza mkewe.
“Ndiyo maana yake, wewe unafikiri mimi napenda kukaa hapa nje?” mkewe alimuuliza.
Baada ya Beka kuambiwa hivyo, alijongea kwenye zulia la mlangoni akalifunua na kutoa funguo, mkewe akapigwa na butwaa.

“Si huu hapa,” alisema Beka akimwonesha mkewe.
“Khaa! Au we ulijua funguo iko hapa nini? Mliwasiliana au mlikuwa wote?” aliuliza Aisha huku akimwangalia mumewe kwa macho yaliyojaa maswali kibao na mshangao juu…
“Hapana, huwa najua wengi wanapoondoka majumbani kama kuna wengine watakuja funguo wanaweka chini ya kapeti, we hulijui hilo?”

“Mimi silijui hilo, nina wasiwasi kwamba huenda alikwambia au mlikuwa pamoja.”
“Hapana mke wangu. Mimi nilijaribu tu. Labda kesi ya msingi kwake iwe ya kumpigia simu halafu hapokei na kama atakuja itabidi nimpe masharti ya jinsi ya kuishi hapa nyumbani kwangu, anatakiwa kufuata sheria za hapa na si vinginevyo anavyotaka yeye.”

Kwa maneno hayo ya mume wake, kidogo Aisha alionekana kuelewaelewa, lakini kabla hajafumbua kinywa, dada yake aliingia…

“Dada ulikuwa wapi na kwa nini nakupigia simu hupokei wakati unajua funguo umezificha mahali?” Aisha alikuja juu…

“Sasa kama funguo ningekuwa nimezificha kweli ningewakuta ndani?”
“Hayo ndiyo majibu yako dada angu?”
“Umeyataka mwenyewe Aisha, kuniuliza .”

Beka alipopata nafasi ya kukaa peke yake alianza kumwona shemeji yake ni tatizo kwani hata kama kweli wanaiba lakini ni kwa nini dada mtu amseme vibaya mdogo wake?
“Kwanza ilitakiwa awe mtulivu sana na mpole maana yeye ni dada mtu, angekuwa mdogo mtu ndiyo anafanya hivyo sawa,” aliwaza sana Beka.
***
Mwezi mmoja na  nusu mbele, siku hiyo shemeji mtu huyo alimtumia meseji shemejiye Beka akimuuliza kama wanaweza kuonana…

“Kuna nini kwani dear?” aliuliza Beka…
“Kuna kitu kizuri sana nataka kukwambia mpenzi wangu jamani.”
“Kama nini?”

“He! Kwani hutaki kukutana na mimi siyo?”
“Niko tayari, ila wewe tu. Ninyetishie basi.”
“Nikunyetishie nini bwana, we tulia. Niambie tuonane wapi?”
“Basi jioni ya saa kumi, palepale pa juzi.”

“Sawa, pale ni mwao najua na mambo mengine nitapata.”
“Acha mambo yako wewe! Mambo kama yapi?”

“Si yale baby bwana na wewe, unajifanya hujui siyo? Unajua kila nikikumbuka tulichoofanya kwenye sita kwa sita kule gesti damu zinanikimbia kwa sana mwilini, natamani tena iwe sasa hivi.”
“Teh! Teh! Teh!” Beka aliishia kucheka kwenye meseji kisha akamwambia shemeji yake…

“Lakini mke wangu unazifuta hizi meseji au unaziacha ili uziangalie kama shoo ya muziki?”
“Aaa mume wangu bwana! Ina maana mimi ni mtoto mdogo kama mkeo?”
***
Muda wa ahadi ulifika, dada wa Aisha alijiandaa akaondoka akiwa ameweka funguo chini ya kapeti kama alivyofanya siku ya kwanza.

“Na leo kama atarudi na kutoziona funguo itakuwa shauri yake...ngoja nikampe raha mumewe, mjini hapa ukilala wenzako hatulazi damu,” dada wa Aisha alijisemea moyoni wakati akielekea katika gesti waliyokuwa wakikutania na Beka.

Akiwa anaelekea huko gesti, alimtumia meseji Beka naye akamwambia achukue chumba akifika atalipa. Baadaye Beka naye alifika, akalipia chumba.

Ndani ya chumba, Beka alipokelewa na mabusu kibao huku shemeji yake huyo akimchagiza na maneno ya nakupenda sana baby, sitaki kukupoteza na mengineyo mengi yenye kujazwa na mahaba.
“Mimi pia baby…mimi pia baby,” ndiyo yalikuwa majibu ya Beka kwa shemeji yake huyo.

“Enhe, katika yote tutakayoyafanya leo au muda huu kwanza nataka uniambie hicho ulichoniitia.”
Shemeji mtu huyo alicheka kwanza kisha akawa siriasi, akafunguka … 
“Baby nimenasa.”

Beka kwanza hakuelewa, akahisi kama alichokisikia amekitafsiri vingine, akamuuliza…
“Unasema?”

“Nasema mwenzio nimenasa ujauzito, maana nimepitiliza.”
“Una maana gani?”
“Nina ujauzito wako bwana, acha mambo yako wewe.”

Itaendelea

Chanzo Globalpublishers







No comments:

 
 
Blogger Templates