Social Icons

Saturday, 12 October 2013

AU YAPITISHA AZIMIO KUHUSU ICC

Kikao cha AU


Viongozi wa Afrika waliokuwa wakikutana mjini Addis Ababa, Ethiopia, wamekubaliana kuwa Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya asihudhurie kesi yake katika Mahakama ya Jinai ya Kimataifa, ICC, ila ikiwa itaakhirishwa.

Katika azimio lao viongozi wa Afrika walisema kuwa kiongozi yeyote wa taifa asitakiwe kuhudhuria mahakama yoyote ya kimataifa wakati yuko madarakani.

Kesi ya Rais Kenyatta ambaye anakabili mashtaka ya uhalifu dhidi ya binaadamu inatarajiwa kuanza mwezi ujao mjini Hague, ingawa ameomba mara kadha kwamba iakhirishwe.

Bwana Kenyatta siku zote amesema kwamba atashirikiana kikamilifu na ICC.

AU inaishutumu ICC kuwa na kigeugeu - kwamba inawashtaki Waafrika na siyo watu wa mataifa ya magharibi.

Hapo awali Waziri Mkuu wa Ethiopia, Hailemariam Dessalegn, alisema kesi za ICC dhidi ya Rais Uhuru Kenyatta na Omar al-Bashir wa Sudan zinaweza kuzuwia juhudi za kuleta amani na mapatano katika nchi zao.

Mkutano umemalizika.

Chanzo:- BBC

PM's SEIZURE HIGHLIGHTS CHAOS IN LIBYA.

Thursday's brief detainment of Prime Minister Ali Zidan has underlined the chaos currently wracking Libya. Analysts say that unless foreign powers offer the government help, the country could become "a failed state."

Libyan Prime Minister Ali Zeidan gives a press briefing on the Libyan Security situation on April 8, 2013 in Tripoli. Gunmen posing as security personnel kidnapped a top aide of Libyan Prime Minister Ali Zeidan, just hours after the premier revealed members of his government had received death threats, a cabinet source told AFP. AFP PHOTO/MAHMUD TURKIA (Photo credit should read MAHMUD TURKIA/AFP/Getty Images)

The seizure of Libyan Prime Minister Ali Zidan from a Tripoli hotel on Thursday morning (10.10.2013) has underlined the political chaos currently wracking the country. The action was swiftly condemned as an "abduction" by the Prosecutor General's office, but, according to news agency AFP, was carried out by a group called the Operations Cell of Libyan Revolutionaries - which is supposed to report to the defense and interior ministries.

Zidan was reportedly held at the Interior Ministry's anti-crime department, even though the prosecutor denied that there was an arrest warrant out for the prime minister, before being released later in the morning, Libya's official LANA news agency reported.

Impossible situation

The move comes during a period of political turmoil in Libya, which was exacerbated by the capture of suspected al-Qaeda operative Nazih Abdul-Hamed al-Ruqai, alias Abu Anas al-Liby, by US special forces on Sunday (06.10.2013). Though many details are still unclear, it seems that Zidan's abduction is a direct reaction to the US raid.

As became obvious when Zidan appeared on the BBC's Newsnight show on Tuesday, the raid on Tripoli by US forces put him in an invidious position. Even as he insisted that "Libya does not surrender its sons," and that Libyan citizens should be tried in Libya, the prime minister called for foreign help to fight militant groups in the country.

Describing how Libya was being used as a base for gun-runners exploiting the country's long, porous borders, Zidan said, "The movement of these weapons endangers neighboring countries too, so there must be international co-operation to stop it."

Equally ambiguous was Zidan's insistence that relations between the US and Libya would not be harmed by the commando raid. "The US was very helpful to Libya during the revolution and the relations should not be affected by an incident, even if it is a serious one," he said at a press conference in Morocco on Tuesday.

Libyan security march towards the parliament building as the surrounding area is closed off in the capital Tripoli, on November 14, 2012, hours before Libyan Prime Minister Ali Zeidan's new cabinet is sworn in following public demonstrations against some of its members. AFP PHOTO/MAHMUD TURKIA (Photo credit should read MAHMUD TURKIA/AFP/Getty Images) 
Factions in the Libyan parliament are not behind Zeidan

"What he's asking for is what every weak government with militants on its soil wants," said Shashank Joshi, analyst at the Royal United Services Institute. "That is, international assistance without any of the domestic political cost or infringements. There is a similar dynamic in Pakistan - they want international help, but on their own terms. They want things like satellite intelligence, drone capabilities, which only America and Europe has."

No bargaining position

Libya's government is in a precarious situation. The leadership is wary of criticizing its most powerful ally, the United States, but is also desperate to placate section of its population, who believe the government tolerated or even colluded in the abduction of a Libyan citizen.

"We will focus on human and citizen rights and on the necessity that he gets a fair trial," Justice Minister Salah al-Marghani told reporters, having won assurances from the US ambassador that al-Liby was being treated humanely. "The government is putting higher national interests in mind."

Those higher national interests are dictated by the fact that armed militias, including Islamic extremists, each control specific areas of the country. In general, the security situation in Libya is close to catastrophic, said Charles Gurdon, director of the security and risk consultancy Menas Associates in the UK. There has there been a series of assassinations of army officers, thought to have been carried out by Islamist extremists and loyalists to former dictator Moammar Gadhafi. In addition, Gurdon pointed out, "The ports in the east are currently under blockade, so Libya is only exporting a fraction of the oil that it produces. And the government is having to bribe militias to open them up."

Zidan: unpopular technocrat

The government's weakness is also political. "The prime minister is very, very unpopular, particularly with the Islamist political groups," Gurdon told DW. "You have a largely technocratic government run by a technocratic prime minister. The parliament chose him, but he wasn't their first choice - he was a compromise candidate between the different factions. The trouble is there isn't anyone to take over. So it's a mess."

"The last thing Libyans want is foreign soldiers on the ground," he concluded. "At the same time, unless there is some sort of foreign help, Libya will become a sort of failed state."

epa03898322 An undated handout picture made available by the US Federal Bureau of Investigation (FBI) on 06 October 2013 shows Nazih Abdul-Hamed al Raghie, also know as Anas al-Liby, who is wanted for Conspiracy to Kill United States Nationals, to Murder, to Destroy Buildings and Property of the United States, and to Destroy the National Defense Utilities of the United States. The suspected leader of the terrorist group al-Qaeda was captured 05 October 2013 in Libya, news reports said. Anas al-Liby, has been sought by the United States since at least the year 2000 when he was indicted in connection with the 1998 bombings of US embassies in Kenya and Tanzania. EPA/FBI BEST AVAILABLE QUALITY -- Black and White only HANDOUT EDITORIAL USE ONLY (zu dpa Gesuchter Al-Kaida-Anführer in Tripolis gefasst vom 06.10.2013)The capture of al-Liby put the Libyan government in an awkward situation

Meanwhile, Zidan's call for international help couldn't have come at a worse time, with foreign military intervention deeply unpopular in both the US and Europe. Any mission would have to be limited. "Basically they need someone to train the national army to disarm the militias and those with connections to al-Qaeda," said Gurdon.

"There are police and army being trained by the British, by the Jordanians, and by others, but the training takes time. And at the moment the government is trying to disarm the militias by buying their arms from them - and of course they're taking the money and not handing over the weapons, or handing over some of the weapons. Even within the army there are members who are really more loyal to their own hometown and their specific leaders."

Lack of trust

The other problem for Western governments is which Libyans to trust. "There's evidence that the US government informed the Libyans about the raid in advance, but it's likely that they would have been afraid of telling more than a few people, or telling them too far in advance, for of leaks." Joshi told DW. "So there's a lack of trust with sensitive intelligence."

"In addition, no one trusts the Libyan justice system to hand over suspects," added Joshi. "It makes it difficult to provide the kind of assistance that Zidan wants. There will be help with border issues, but the list of areas of where Libya needs help is a very long one."

Source:- Dw.de


LOCAL CONFLICT, TRIBAL FEUDS PERVADE LIBYA.

Ever since its revolution, Libya has been riddled with tribal conflict. The state remains powerless in the face of weapon proliferation and violence. Societal fragmentation seems inevitable.

 Libyan security gather in the capital Tripoli on September 21, 2013. (Photo: MAHMUD TURKIA/AFP/Getty Images)

At the entry to the village of Bani Walid, someone scrawled "Allah, Muammar, Libya and nothing else" on a wall. It's a battle cry among Gaddafi supporters and one that's been frowned upon ever since the rebels' victory. The residents of the mountain village, which is roughly 170 kilometers (106 miles) south of the capital Tripoli, look upon them as losers of the revolution. The privileges of the once mostly Gaddafi-loyal residents have vanished since his downfall.

The Warfalla, Libya's largest tribe, play a dominant role in Bani Walid. Along with the Qadhadhfa, former ruler Muammar al-Gaddafi's tribe, the Warfalla used to be especially powerful. By way of tribal relations, Bani Walid is connected to the former Gaddafi stronghold Sirte on the Mediterranean coast and to Sebha, capital of the country's southwest region. In all three towns, the majority supported the regime in 2011.

Bullet holes on a door in Bani Walid
. (Photo: Karlos Zurutuza / DW)Bullet holes are just one sign of destruction in Bani Walid

Destruction can be seen everywhere in Bani Walid. In 2011, NATO troops bombed the town, and after a further state-ordered military attack in October 2012, Bani Walid looks like a ruinous fort. It became a target because of tensions with the port city of Misrata, a stronghold of Gaddafi's opponents.

Revenge, retribution and tribal wars

The conflict between Misrata and Bani Walid is just one example of local rivalries all across the country. Most of them originate where armed ethnic groups fight for influence, land and resources. The interim government is mostly powerless to stop such disputes. One reason for that is the state's attempt to integrate whole rebel groups into the army. Many of those groups prioritize the interests and commands from their tribes over the national good.

What begins as a skirmish often turns into days of battles and, ultimately, the displacement of the weaker group. Tribal feuds have existed for centuries. But Gaddafi aggravated existing tensions by favoring certain tribes and villages and resettling certain ethnic groups.

Security forces are positioned outside the court in Tripoli during the pre-trial hearing of Libya's ex-intelligence chief Senussi Baghdadi al-Mahmudi. (Photo: MAHMUD TURKIA/AFP/Getty Images) Guns and violence are omnipresent in Libya

After Gaddafi's ouster and death in October 2011, the rebels began seeking retribution for war crimes. All 30,000 residents of the former Gaddafi-stronghold Tawergha were arrested, chased away or killed by rebel troops from the neighboring Misrata. The city has been deserted ever since.

Settling scores from 40 years of dictatorial rule keeps the cycle of violence alive. Some of the landowners whose land was confiscated by Gaddafi are resorting to violence to reclaim their estates. Tribes like the Awlad Suleiman, which faced repression under the dictator, are now pushing to the fore.

Racism and sarcasm

Many people in the town of Sebha feel threatened by the uprising. "Returnees and intruders control the city council and blackmail the government," landowner Hussein Mohamed, who is among the wealthy in the area, complains. He doesn't have much sympathy for the Awlad Suleiman, whom he considers rioters. But even they, he says, are better than another group known as the Toubou.

Members of the Toubou ethnic minority live in Chad, Niger and Libya and are considered by most Libyans to be invaders. Even those who were born in Libya can't escape this stigma. "Disposition is hereditary - a thief can only beget other thieves," Hussein Mohamed says dismissively of the minority group. Racism is rampant across Libya, especially towards African migrants and the black Toubou.

Tubu and Tuareg honoraries and military members in Murzuq. (Photo: Valerie Stocker/ DW)Toubou and Tuareg feel ignored by Libya's government

"My skin color is supposed to determine whether I'm from here?" Sidi Kella, a tradesman from Murzuq, asks incredulously. "I'm more Libyan than many Arabs!"

Others use sarcasm. "Hey, you Chadian mercenary!" quip two young men as they greet each other on the street.

The Toubou expect little from their fellow citizens and from the state. Mostly, they rely on the military power they gained in 2011. "You could be as revolutionary as you wanted, but without a Kalashnikov, you were nothing," recalls Hassan Shaha, a fighter in Ubari, located southwest of Sebha.

The time of the revolutionaries seems to be over, but the era of prevalent arms isn't. In Sebha, there are bloody clashes between members of the Toubou and of the Awlad Suleiman on a regular basis.

Minorities and regional autonomy

The minorities - Berbers, Tuareg and Tubu - want more say in their fates and are increasingly threatening violence if they continue to be ignored. Their representatives have already quit parliament in anger after no agreement could be reached on Libya's new constitution.

In Ghat, a city in the western Fessan region, the Libyan Tuareg tribes recently held an assembly and set up a committee to represent their interests. "Our demands are humble," Ghat's mayor Mohamed Abdelqader says. "We call upon the state to support our culture and language, to give us more state jobs and to put money into developing our region. But no one in Tripoli cares for the rest of the country." A Berber activist claims that plans are being made to create a minority coalition to oppose the government.

In eastern Libya, a protest movement is pushing for the independence of the region. Protestors challenge the government by blocking oil ports, and there are reports that similar campaigns are underway in Fessan.

Local leaders in Fessan are asking where the country's patriots are, but the latter, too, are now largely given over to their own tribes' interests.

Source:- Dw.de

US AIR FORCE GENERAL MICHAEL CAREY IN CHARGE OF ICBM MISSILES FIRED FOR ALLEGED MISCONDUCT.

Just two days after a Navy admiral was sacked, the Air Force has fired the general in charge of its nuclear missiles. Personal misbehavior in connection with alcohol abuse has been cited as the cause.

A surface-to-surface missile . Photo Reuters

The US Air Force has removed Major General Michael Carey, a 35-year veteran, from his command of 20th Air Force, responsible for all 450 of the service's intercontinental ballistic missiles (ICBM). The move comes after an investigation revealed alleged "personal misbehavior."

The Air Force did not say what Carey was alleged to have done wrong, but two officials with knowledge of the investigation told the Associated Press that it was linked to alcohol use. Carey is to be reassigned pending the outcome of an investigation.

On Wednesday the Navy announced that Vice Admiral Tim Giardina, the second-in-charge at US Strategic Command, was fired amid an investigation for allegedly using counterfeit chips at a casino in Iowa. He was demoted from three- to two-star rank and reassigned to a Navy staff job until the investigation was completed.

The most senior nuclear commander, Air Force General Robert Kehler, called the Carey and Giardina matters "unfortunate behavioral incidents," but he did not discuss details.

Kehler added: "I still have 100 percent confidence that the nation's nuclear
deterrent force is safe, secure and effective."

The US has been shrinking the size of its nuclear arsenal for many years. It is made up of long-range missiles on board submarines, long-range bombers and ICBMs. As of October 1 the US had 1,688 deployed strategic nuclear warheads, which Washington is obliged to reduce to 1,550 by 2018 under the New START treaty with Russia.

Source:- Dw.de

TYPHOON NARI SWEEPS THROUGH PHILIPPINES.

Heavy flooding and strong winds from Typhoon Nari have caused widespread damage and claimed lives in the Philippines. The storm is now heading toward Vietnam.

 Vehicles maneuver through flood waters on a road in the northern Philippines October 12, 2013. Typhoon Nari swept across the farming region north of Manila, killing eight people and leaving two million others without electricity. AFP PHOTO / Jay DIRECTO (Photo credit should read JAY DIRECTO/AFP/Getty Images)

Emergency personnel worked on Saturday to restore power to an estimated two million people in the northeast Philippines. Winds of up to 150 kilometers per hour (93 miles per hour) toppled pylons and trees and ripped roofs off buildings overnight after the storm made landfall in the province of Aurora, which lies less than 200 kilometers (124 miles) northeast of the capital Manila.

"A lot of areas are still flooded," said Eduardo del Rosario, head of the National Disaster Risk Reduction and Management Council said.

The governor of neighboring Bulacan province - Wilhelmino M. Sy-Alarado - told the Associated Press news agency that more than 20 villages were under water, some up to 2 meters (6.6 feet). Roughly 10,000 hectares (24,700 acres) of rice and vegetable farms had been damaged, he added.

Officials evacuated several thousand people before the category one typhoon made landfall. Nevertheless, the storm claimed over a dozen lives. At least 5 people were killed when trees crashed into their homes, according to the National Disaster Risk Management Office. A landslide and high waters were responsible for several other deaths, according to the same officials.

Typhoon Nari is now headed west toward Vietnam.

Source:- Dw.de


MASS EVACUATIONS AS SUPER CYCLONE PHAILIN NEARS EAST INDIA.

Hundreds of thousands of people have fled their homes in India as Cyclone Phailin barreled toward the country's east coast. Phailin has filled nearly the entire Bay of Bengal, an area the size of France.

 A big wave smashes into a breakwater at a fishing harbour in Jalaripeta in the Visakhapatnam district in the southern Indian state of Andhra Pradesh October 11, 2013. Tens of thousands fled their homes in coastal areas of eastern India and moved to shelters on Friday, bracing for the fiercest cyclone to threaten the country since a devastating storm killed 10,000 people 14 years ago. REUTERS/Stringer (INDIA - Tags: DISASTER ENVIRONMENT)

The Indian Meteorological Department issued a red alert on Saturday, warning of the "very severe" cyclone's impending landfall, while authorities continued to evacuate villages along the coast in the states of Andhra Pradesh and Orissa.

So far, more than 400,000 people have fled to government shelters, according to Marri Shashidhar Reddy, vice chairman of the National Disaster Management Authority.

"This is one of the larges evacuations undertaken in India," Reddy said.

The Indian Meteorological Department has forecast winds of up to 220 kilometers per hour (137 miles per hour), warning of extensive damage to mud houses, power and communication disruptions, and flooding of rail tracks and escape routes.

"No one will be allowed to stay in mud and thatched houses in the coastal areas," said Surya Narayan Patro, Orissa state's top disaster management official.

'Super cyclone'

Meanwhile, the US Navy's Joint Typhoon Warning Center said that Phailin's winds could reach 315 kilometers per hour. The London-based Tropical Storm Risk classified Phailin as a category 4, which designates a "super cyclonic storm."

"If this is not a record it's really, really close," hurricane researcher Brian McNoldy, with the University of Miami in the US, told the Associated Press. "You really don't get storms stronger than this anywhere in the world ever. This is the top of the barrel."

The 1999 Orissa cyclone, similar in strength to Phailin, killed more than 8,000 people. Authorities say they are better prepared this time.

"With the horrendous experience of 1999 still haunting them, no one wants to take anything for granted," retired government officer Yudhistir Mohanty told the AFP news agency.

Source:- dw.de


KERRY, KARZAI EXTEND TALKS ON US-AFGHAN PARTNERSHIP.

Afghanistan's President Karzai has extended talks with US Secretary of State Kerry to negotiate a pact determining how many US troops stay in the country after 2014. A decision must be made by the end of the month.

US Secretary of State, John Kerry (CL) meets with Afghan President Hamid Karzai (Photo: JACQUELYN MARTIN/ AFP/Getty Images)

Afghan President Hamid Karzai's spokesman, Aimal Faizi, told reporters on Saturday that "there are still issues we [the US and Afghanistan] are finalizing ... therefore, there is a need for a third round of talks this evening."

Karzai and US Secretary of State John Kerry met Friday (pictured above) for their first round of talks. They appeared to have reached an agreement on the first of the two sticking points: a US request to run independent counterterrorism missions on Afghan territory.

The second sticking point was to reach terms for a US military presence in Afghanistan after 2014. US President Barack Obama had told Karzai last June that if there was no agreement by October 31 on the terms for keeping a residual military presence in Afghanistan, the US could pull out all of its forces by the end of 2014 in an outcome known as the "zero option." The Afghan president has signaled a preference to wait for next spring's elections to decide.

"We will try to see if we can make a little more progress, which we have been doing," Kerry told reporters and US Embassy staff on Saturday.

Another contentious point between the two governments is reportedly Washington's refusal to guarantee the country protection from intervention by foreign forces, primarily from Pakistan.

source:- dw.de

MWAKYEMBE AZITAKA BENKI KUISAIDIA BANDARI.


Dar es Salaam. Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe, ameziomba taasisi za kibenki nchini, kutoa huduma kila siku, ili kupunguza foleni ya meli zilizopo katika Bandari ya Dar es Salaam.

Kauli hiyo ya Dk Mwakyembe inatokana na kumalizika kwa mgomo wa malori uliodumu kwa zaidi ya siku tatu na kusababisha meli zaidi ya 27 kukwama katika foleni ya kushusha shehena.

Dk Mwakyembe alisema hayo jana wakati akiipokea meli kubwa yenye zaidi ya mitaa 250. Alisema ni vyema benki zikafanya kazi kila siku ili kuongeza ufanisi wa huduma katika Bandari ya Dar es Salaam.

“Taasisi za kibenki tumeziomba kusogeza huduma hapa bandarini na wafanye kazi hadi mwishoni mwa wiki ili kuendelea kupunguza meli zinazosubiri kushusha mizigo. Watanzania tuache kulala tuko nyuma, tuchape kazi hata Jumapili tuisogeze mbele nchi yetu,” alisema Dk Mwakyembe.

Alisema kuwasili kwa meli hiyo kubwa kunafungua milango kwa meli zingine za aina hiyo.

Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Madeni Kipande, alisema wamefanya juhudi za makusudi kuileta meli hiyo yenye uwezo wa kubeba kontena zaidi ya 4,500 ili kuonyesha uwezo wa bandari hiyo katika Ukanda wa Afrika Mashariki.

Alisema wanaendelea kuhakikisha kuwa bandari hiyo inapiga hatua zaidi kwa kutoa huduma bora na kwa ufanisi zaidi kwa kupunguza muda wa upakuaji wa mizigo kwa haraka zaidi.

“Tutafanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha meli kuwa zilizopo katika foleni zinaondoka kwa wakati. Tmejipanga kikamilifu kuhakikisha kuwa bandari hii inaendelea kuwa bora,” alisema Kipande.

Kwa upande wake, Nahodha wa meli hiyo ambaye ni Mtanzania, Abdull Mwingamno, alisema kazi ya kuileta meli hiyo nchini kutoka Ruanda, Angola ilikuwa rahisi.

“Namshukuru Mungu kuwa nimeifikisha salama meli hii na najua kufika kwa meli hii nchini kwetu kutazifanya na meli kubwa zaidi ya hii kuja nchini kwetu,” alisema Mwingamno.

Chanzo:- Mwananchi.


SABABU ZA MWALIMU KUNG'ATUKA KATIKA UONGOZI.


Kwa mujibu wa wajuzi wa mambo Nyerere aliweka wazi dhamira yake hiyo mwishoni ya miaka ya sabini, ambapo alibainisha wazi kuwa angestaafu mwaka 1980.

Lakini kabla ya kuikamilisha dhamira yake, nchi ya Tanzania ikaingia kwenye vita kati yake na Uganda.

Vita hiyo ilikuwa kati ya mwaka 1978 na 79. Mwalimu Nyerere akiwa Amiri Jeshi Mkuu aliongoza vita hiyo hadi pale Tanzania ilipoibuka mshindi na kuikomboa ardhi yao, ambayo Uganda ilikuwa na mpango wa kuitaifisha.

Kutokana na ukweli kuwa hali ya nchi haikuwa nzuri kiuchumi na hata kiusalama, hivyo akaombwa aendelee na uongozi kwa miaka mitano zaidi.

Na hapo ndipo alipoendelea na uongozi hadi Novemba 7, 1985, alipoamua kung’atuka rasmi katika nafasi zake zote za uongozi ndani ya Chama na Serikali.

Tukio la kung’atuka kwake kutoka katika nafasi zake hizo limekuwa likitafsiriwa kwa mitazamo tofauti tofauti, licha ya ukweli kuwa hiyo haikuwa mara ya kwanza kwake kufikia uamuzi huo.

Awali alishawahi kuachia ngazi katika madaraka yake ya Uwaziri Mkuu mwaka 1962, ili aende akaimarishe chama chake cha TANU.

Mwalimu Nyerere alipoeleza nia yake ya kung’atuka madarakani kama rais na baadaye kama mwenyekiti wa CCM, wananchi wengi sana walionyesha hofu kubwa, na hata baadhi yao walijaribu kumzuia asiondoke madarakani.

Licha ya ukweli huo lakini bado Mwalimu Nyerere alikuwa na sababu zake, zilizomsukuma hadi kufikia uamuzi wake huo.

Je, ungependa kufahamu sababu hizo?

Sababu kuu iliyomfanya baba huyo wa Taifa la Tanzania ang’atuke madarakani, ni pale tu alipoona amekwisha ijenga misingi muhimu na imara.

Misingi hiyo ni pamoja na umoja, amani, upendo, haki, usawa demokrasia uongozi wa nchi na maenedeleo katika nyanja za elimu, uchumi na siasa.

Chanzo:- Mwananchi.

ICC: KESI YA SENUSSI IFANYIKE LIBYA



Mahakama ya kimataifa ya jinai, ICC, imeamua kuwa aliyekuwa mkuu wa ujasusi wakati wa utawala wa marehemu Muamar Gadaffi, Abdullah al-Senussi, afunguliwe mashtaka nchini Libya.

Uamuzi huu una maana kuwa ICC haitaendelea kumtaka tena Bwana Senussi kwenda Hague kwa kesi dhidi yake.


Bwana Senussi alikabidhiwa na Mauritania kwa Libya baada ya kukamatwa nchini humo mwaka jana.
Senussi aliyekuwa mkuu wa ujasusi alitakikana na mahakama ya ICC kwa uhalifu dhidi ya binadamu , makosa aliyoyafanywa wakati wa mapinduzi ya kiraia dhidi ya Gaddafi.

Mahakama ya ICC kawaida haiendeshi kesi dhidi ya mshukiwa ikiwa kuna dalili kwamba watatendewa haki nchini mwao.

Aidha katika taarifa yake mahakama hiyo imesema kuwa uamuzi huo hauna uhusiano wowote na kesi dhidi ya mwanawe marehemu Gaddafi,Saif al-Islam Gaddafi anayetakikana na mahakama hiyo.

Islam pia alishtakiwa kwa makosa ya uhalifu wa kivita na alishitakiwa pamoja na watu wengine 36.

Saif Gaddafi anazuiliwa na kundi la wapiganaji wa kiisilamu mjini Zintan. Mwezi jana wapiganaji hao, walikataa kumkabidhi Seif kwa serikali kuweka kufikishwa mahakamani pamoja na Senussi .


Chanzo:- BBC

DR. MAHANGA, MEYA SLAA WAVUTANA.


Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dk Makongoro Mahanga amembeza Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa kwa hatua yake ya kumshambulia kupitia vyombo vya habari akibainisha kuwa busara yake ni ndogo kama umri wake.

Dk Mahanga alimbeza Silaa juzi, wakati akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu baada ya kuhojiwa ambapo alibainisha zaidi kuwa, busara na umri alionao vinamwongoza asilumbane na viongozi wenzake kwenye vyombo vya habari.

“Mimi nina miaka 58 yeye ana miaka 31, busara zetu ni tofauti sana hata kwenye malumbano, ingawa mimi nina cheo kidogo kwenye chama ukilinganisha na yeye, mimi ni mbunge tu CCM, mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Mkoa wa Dar es Salaam na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa chama, wakati yeye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM,” alisema Dk Mahanga.

Alisisitiza kuwa busara aliyonayo meya huyo ndiyo iliyomfanya amfananishe na Punda ndani ya Baraza la Madiwani waliokuwapo kwenye kikao hicho na waandishi wa habari waliohudhuria.

Kwa upande wake, Meya Silaa alibainisha kuwa tuhuma dhidi ya Dk Mahanga zilitolewa ndani ya Kikao cha Baraza la Madiwani Manispaa ya Ilala, Dar es Salaam, ambapo kwa mujibu wa tangazo la Serikali namba 11 la Aprili 16, mwaka 2004, kanuni za kudumu za halmashauri hiyo sehemu ya (iii) 24 inakataza suala lililojadiliwa kwenye kikao hicho kuhojiwa nje ya hapo na chombo chochote ikiwamo mahakama.

“Kanuni hiyo inaeleza kutakuwa na uhuru wa kutoa mawazo wakati wa majadiliano katika mikutano ya halmashauri na uhuru huo hautaweza kuhojiwa katika mahakama yoyote au popote nje ya mkutano wa halmashauri,” Silaa alinukuu kanuni hiyo.

Oktoba 3, mwaka huu Meya Silaa, alikaririwa na vyombo vya habari akiwa kwenye kikao cha Baraza la Madiwani Manispaa ya Ilala,Dar es Salaam, akilaani vikali migogoro ya kisiasa isiyo na tija kwa wananchi ukiwamo uliosababishwa na barua iliyoandikwa na Mbunge wa Segerea ambaye ni Dk Mahanga.

Alidai kuwa barua hiyo ilisababisha aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Gabriel Fuime kusimamishwa kazi bila kufuatwa taratibu za utumishi hivyo kutia doa utumishi wake wa muda mrefu.

Silaa alisisitiza kuwa, Dk Mahanga hakujali msaada wa Fuime ambaye aliutoa jimboni kwake wakati wa Uchaguzi Mkuu 2010, badala yake kuna barua ya siri iliyoandikwa kwenda Tamisemi ikimtuhumu Fuime na Silaa wakidaiwa kuhusika na tuhuma mbalimbali za ubadhirifu.

Ilidaiwa kuwa kutokana na tuhuma hizo, Fuime alisimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi dhidi yake ambapo miongoni mwa tuhuma hizo ni pamoja na kushindwa kusimamia mapato ya halmashauri hiyo na ukodishaji unaotia shaka katika Soko la Samaki Feri.

Chanzo:- Mwananchi


JK: MA-DC MUWE NA AJENDA.


RAIS Jakaya Kikwete, amewataka wakuu wa wilaya na wabunge kubuni mipango kazi na ajenda za kusimamia maendeleo kama namna ya uhakika zaidi ya kutoa uongozi kwa jitihada za wananchi kujiletea maendeleo.

Rais Kikwete alitoa kauli hiyo juzi alipozungumza na viongozi wa mkoa wa Pwani kwenye Hoteli ya Oceanic Bay mjini Bagamoyo wakati akikamilisha na kujumuisha ziara yake ya siku sita ya kukagua na kuzindua shughuli na miradi ya maendeleo katika mkoa huo.

Alisema ukosefu wa mipango ya kazi na ajenda ya utendaji unasababisha wakuu wa wilaya wengi kuendesha shughuli zao kwa matukio tu na kutegemea ratiba za ziara za wakubwa zao wa kazi.

Alisema anatamani kazi yake ingekuwa inampa uhuru wa kuingia wilayani na kukagua mipango kazi ya mkuu wa mkoa bila kujulikana kama ameingia katika wilaya hiyo.

“Maendeleo ya wananchi ndiyo shughuli yenu kubwa ya uongozi. Hivyo, ni lazima muwe na mipango kazi ya maendeleo ya wananchi. Na kwa sababu wakati mwingi hatuna mipango kazi ya shughuli za kila siku za maendeleo ya wananchi basi tunafikia hatua ya sisi viongozi kuanza kugombea mafaili.

“Kwa hakika, natamani kuwa ningekuwa na nafasi na uhuru wa kuchomoka bila kugundulika na kuingia katika wilaya kukagua mipango kazi ya mkuu wa wilaya bila kujulikana kama nimeingia katika wilaya hiyo.

Na kwa sababu wengi wetu hatuna mipangokazi na ajenda ya kazi ya maendeleo ya wananchi tunaishia katika kwenda na matukio, akifika Waziri Mkuu tunaingia katika ratiba yake, akifika fulani tunapata ajenda ya kazi,” alisema.

Rais Kikwete alisema endapo viongozi hawatakuwa na ajenda ya maendeleo hakuna jambo lolote la maana litafanyika.

“Bila nyie viongozi kuwa na ajenda ya maendeleo, hakuna jambo lolote la maenddeleo ambalo litafanyika na mtamaliza muda wenu na kuondoka madarakani bila kuacha lolote la kukumbukwa na wananchi,” alisema.

Chanzo:- Tanzania Daima.

MEYA MSTAAFU ASHINDA KESI YA MAUAJI.

VILIO vya furaha jana vilitawala katika Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza baada ya aliyekuwa Meya wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Leonard Bihondo na wenzake watatu kuachiwa huru katika kesi ya mauaji ya aliyekuwa Katibu wa CCM Kata ya Isamilo, Bahati Stephan iliyokuwa ikiwakabili.

Akisoma hukumu hiyo ya shauri namba 79 la mwaka 2011, Jaji Aisheri Sumari alisema kuwa ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri umeshindwa kumtia hatiani mshitakiwa namba moja katika kesi hiyo, Jumanne Oscar ambaye alituhumiwa kutekeleza mauaji hayo kwa kumchoma Bahati kisu katika ziwa lake la kushoto.

Akisoma maelezo ya shahidi namba 16 na 18 ambao walikuwa ni askari polisi waliokabidhiana mtuhumiwa namba moja, alisema kuwa ushahidi wao ulikuwa na mkanganyiko hivyo kutoa faida kwa washitakiwa.

Jaji Sumari alisema kwa maelezo yao, shahidi namba 16 anasema kuwa alipelekwa mahabusu na shahidi namba 18 kumchukua mshitakiwa namba moja, kisha kmpeleka kwa RCO Muna kuchukuliwa maelezo.

Aliongeza kuwa shahidi namba 18 katika ushahidi wake alisema kuwa tangu alipomkabidhisha mtuhumiwa kwa OCD siku ya tukio, hajawahi kurudi wa kushughulika na kesi hiyo hadi alipokwenda kutoa ushahidi mahakamani.

“Mkanganyiko huo ulitakiwa kuondolewa na Malingumu ambaye mpaka sasa ni askari, lakini upande wa Jamhuri wameshindwa kushughulika na hilo, hivyo kushindwa kuamini maelezo ya ushahidi,” alisema.

Jaji Sumari alisema kuwa pande wa mashitaka haukutaka Malingumu kufika mahakamani kuthibitisha mtuhumiwa aliyekabidhiwa na shahidi namba 18 (Sostenas) kama ndiye mshitakiwa namba moja.

Alisema kuwa uwezekano wa kuwachanganya washitakiwa ni mkubwa kutokana na ushahidi uliotolewa na shahidi namba 16 na 18, kwa sababu kama mshitakiwa namba moja ndiye aliyekamatwa ziwani, haoni kwanini awe na majeraha wakati shahidi namba 7 na namba 2 walimkabidhi mtuhumiwa kwa askari bila majeraha yoyote.

Kufuatia maelezo hayo, Jaji Sumari alisema kuwa kuna mkanganyiko mkubwa upande wa mashahidi wa Jamhuri juu ya mtu aliyechukuliwa na polisi na mtuhumiwa aliyetolewa ziwani.

“Hapa kuna maswali mengi ya kujiuliza, kwanini upande wa Jamhuri hawakuita gwaride la utambuzi kwa sababu wananchi ndio waliomkamata mtuhumiwa ziwani na kumkabidhi kwa askari wakati kesi hiyo imechukua muda mrefu?” alihoji.

Alisema kuwa anakubaliana na hoja za wakili wa mshitakiwa wa kwanza, Stephan Magoiga kuwa ushahidi unaotolewa hapo ni utambuzi wa mahakamani na si eneo la tukio ambapo mahakama haiwezi kumtia hatiani mshitakiwa huyo.

Kuhusu upande wa utetezi wa washitakiwa, Jaji Sumari alisema kuwa mtuhumiwa namba moja ambaye alikuwa na kesi ya kujibu aliuchambua vizuri ushahidi uliotolewa na shahidi namba 16 na 18 na kudai kuwa umeonyesha wazi mkanganyiko kutokana na vielelezo vya nguo ambavyo alikuwa amevaa.

Alisema kuwa mashahidi hao walimtambua kwa suruali aliyokuwa amevaa aina ya jinzi ambapo kielelezo kilichofikishwa mahakamani ni cha suruali ya khaki ambayo ilikuwa na damu.

Kutokana na maelezo hayo, Jaji Sumari alisema kuwa ameridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri kuwa hauwezi kuwatia hatiani washitakiwa wote wanne, hivyo akawaachia huru.

Chanzo:- Tanzania Daima.

MAGUFULI AZIDI KUWEKWA KITANZINI.


WAMILIKI wa malori nchini wamesema kuwa serikali imepata hasara ya sh bilioni 20 hadi 30 kufuatia kusitishwa kwa huduma ya usafirishaji mizigo kwa madai ya kulinda barabara zisiharibike.

Mbali na hasara hiyo, wamiliki hao wamemuomba Rais Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuhakikisha wanamchukulia hatua za kinidhamu Waziri wa Ujenzi, John Magufuli kutokana na kupotosha suala hilo kwa umma.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, kwa niaba ya wenzake, Azim Dewji ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya usafirishaji ya Simba alisema kuwa serikali imepoteza mapato hayo kutokana na uongo wa Magufuli.

Dewji alisema kuwa hasara waliyoipata wamiliki wa malori hayo ni kubwa na sasa wapo katika kufanya mahesabu ili kuibaini ikiwa ni pamoja na kumchukulia hatua za kisheria Dk. Magufuli kwa kumfungulia mashitaka.

“Serikali tu imepoteza zaidi ya sh bilioni 20 na mama lishe nao wameshindwa kufanya kazi zao huko bandarini. Ni ajabu kuwa na kiongozi anayetesa Watanzania kutokana na uongo wake,” alisema.

Dewji alisema kuwa wamiliki wa malori wamekuwa na mchango mkubwa katika uchumi wa nchi, na kwamba wametoa ajira kubwa kwa Watanzania.

Alisema kuwa kwa kipindi cha siku moja malori zaidi ya 1,000 yamekuwa yakifanya safari nchini na kuingiza fedha nyingi serikalini.

Dewji aliongeza kuwa ni muhimu Dk. Magufuli akatoa maneno yenye hekima na busara, na sio kutumia mabavu na kutoa kejeli dhidi ya Watanzania.

Alisema kuwa Magufuli amewadhalilisha kwa kudai kwamba wamekuwa wakitoa rushwa kwa wafanyakazi wa mizani jambo ambalo halina ukweli wowote.

“Hivi kama sio uongo na upotoshaji unaofanywa na kiongozi huyo ni nini? Ni mfanyabiashara gani aliye tayari kutoa rushwa ya fedha kwa vituo vya mizani zaidi ya 14 vilivyopo kati ya Dar es Salaam hadi Tunduma asiyeangalia faida?” alihoji.

Alishauri kuwa ni vyema waziri huyo akatumia vyombo vya dola kufanya uchunguzi juu ya masuala mbalimbali yanayohusu barabara kuliko kutoa kauli za ubabe na kupotosha.

Kwa mujibu wa Dewji, Waziri Magufuli amekuwa na chuki na wamiliki wa malori baada ya kubaini kuwa walikutana na Kamati ya Miundombinu kipindi cha Bunge na kueleza changamoto zinazowakabili.

Waziri Mkuu Pinda juzi aliagiza wamiliki wa malori kuyaruhusu yasafirishe mizigo kwa utaratibu wa zamani badala ya ule wa Magufuli wa kanuni namba 7 (3) ya Sheria ya Usalama Barabarani ya mwaka 2001.

Sheria hiyo inayataka malori yote yanayozidisha uzito uliopo ndani ya asilimia tano kupunguza mzigo, kupanga mzigo upya au kulipia uzito uliozidi mara nne ya tozo ya kawaida.

Chanzo:- Tanzania Daima.

ZITTO AFICHUA NJAMA CHAFU.



NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe amesema kuna njama inayofanywa na wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutaka mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya usiishe ili wajiongezee muda hadi mwaka 2017.

Zitto ambaye pia ni mbunge wa Kigoma Kaskazini, alisema kuwa lengo la wabunge hao ni kutaka muda wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 usogezwe mbele hadi 2017 ili waendelee kukaa madarakani.

Alisema kuwa CHADEMA haitakubali uvunjwaji wa aina yoyote wa katiba, na hivyo kumtahadharisha Rais Jakaya Kikwete kutothubutu kukubaliana na fitna hizo.

Madai ya Zitto yaliwahi pia kutolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba ambaye alisema kuwa CCM wanataka kukwamisha mchakato wa katiba makusudi ili kutengeneza sababu ya kuongeza muda wa Rais Kikwete kubaki madarakani kwa miaka miwili zaidi.

Prof. Lipumba alisema kuwa hoja ambayo CCM wanataka kuitumia kukwamisha mchakato huo, ni muundo wa serikali ambapo dakika za mwisho wanataka kukubali serikali tatu kisha watumie kisingizio cha uundwaji wa taifa la Tanganyika kuchelewesha katiba mpya.

Akihutubia mikutano mbalimbali ya hadhara katika Jimbo la Bukene mkoani hapa, ukiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya ujenzi wa chama katika Kanda ya Magharibi jana, Zitto alisema hata vurugu zilizotokea bungeni hivi karibuni na Naibu Spika Job Ndugai, kuruhusu askari waingie ndani ya Bunge kuwakamata na kuwapiga wabunge wa upinzani, ilikuwa ni sehemu ya mpango huo wa kutaka kusogezwa mbele kwa muda wa wabunge kutoka madarakani.

Zitto alifafanua kuwa hoja inayojengwa na wabunge hao ambao wameshaanza kuipenyeza kwa ajili ya kumfikia Rais Kikwete, ni kwamba kama katiba mpya itapatikana kwa wakati huu, muda wa kujiandaa na uchaguzi wa mwaka 2015 utakuwa hautoshi.

“Hawa ni wabunge waroho wa madaraka, hawajafanya jambo lolote jema katika majimbo yao, na sasa wanajua hawawezi kurudi ndiyo maana wanataka muda usogezwe na wao waendelee kulipwa mshahara na posho.

“Sisi CHADEMA tunasema hilo hapana, hatuwezi kukubali uchaguzi usogezwe kwa miaka miwili, na namuonya Rais Kikwete asithubutu kuingia katika mkenge huo unaowahusisha baadhi ya mawaziri,” alisema.

Aliongeza kuwa wananchi waliwachagua wabunge wao kuhudumu kwa kipindi cha miaka mitano, na kwamba kuwe na katiba mpya au isiwepo ni muhimu uchaguzi kufanyika ili wale walioshindwa kuwajibika wakae pembeni.

Zitto alisema CHADEMA inatoa kauli hiyo ili wananchi wajue mkakati huo, na washiriki kuupigia kelele, kwa kile alichoeleza kuwa mipango hiyo imeshaanza jijini Dar es Salaam na Dodoma.

Kwa mujibu wa Zitto, baadhi ya mawaziri wanataka kutumia nafasi ya kuwa karibu na rais ili kumshawishi akubali mkakati huo, kwa kumueleza kuwa hali hiyo itamjengea heshima na kumbukumbu ya kuiachia nchi katiba iliyo bora.

Avunja ngome ya CCM

Katika hatua nyingine, Zitto ameitikisa ngome ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora, Hassan Wakasuvi.

Dalili ya ngome hiyo kutikiswa ilianza kuonekana mapema wiki hii wakati viongozi wa CHADEMA Wilaya ya Uyui walipokuwa wakifanya maandalizi ya mkutano katika Kata ya Mabama, ambako ni nyumbani kwa kigogo huyo.

Baada ya kutangazwa kuwapo kwa mkutano wa CHADEMA katika kata hiyo, gazeti hili lilishuhudia jitihada mbalimbali za viongozi wa CCM zikifanyika, ikiwemo kuweka bendera mpya kila baada ya nyumba mbili, huku zile nyumba za wakazi wasiokuwa wafuasi wa chama hicho, zikiwekwa barabarani.

Baadhi ya wakazi wa kata hiyo na maeneo mengine ya jirani ambao walijitokeza kumsikiliza Zitto, walieleza kuwa baadhi ya nyumba zilizowekwa bendera wakazi wake walitishiwa kufanyiwa hujuma kupitia ofisi ya mtendaji wa kata hiyo endapo wangekataa.

“Unaona bendera zote ni mpya, hapa tumewachoka, na sasa wanatumia vitisho kutaka kuweka bendera zao kwenye nyumba zetu,” alisema mmoja wa wakazi hao ambaye hakutaka kutajwa jina.

Hata hivyo, mkutano wa Zitto nusura uingie dosari baada ya msafara wake kuchelewa kufika katika Kata ya Mabama, kisha mtu aliyejitambulisha kama ofisa mtendaji wa kata hiyo, kuwataka wananchi watawanyike kutoka katika uwanja wa mkutano.

Lakini wananchi hao hawakukubaliana na agizo hilo na kuahidi kumsubiri Zitto ambaye aliwasili katika eneo la mkutano saa 12:47 jioni na kuwahutubia hadi saa moja na robo usiku.

Kabla ya kuhutubia mkutano huo, Zitto aligawa kadi kwa wanachama wapya waliotoka CCM na kuwataka wasiogope vitisho vyovyote vinavyofanywa na viongozi wa chama hicho.

Alisema CCM imeua njia ya reli iliyokuwa ikiwasaidia wakazi wa Mabama kufanya shughuli za kila siku za kujipatia kipato.

Hata hivyo, Wakasuvi alikanusha chama chake kujihusisha na vitendo vya kuwatisha wananchi, akisema kuwa wao wanatumia nguvu ya hoja.

Chanzo:- Tanzania Daima


 
 
Blogger Templates